ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

Ufisadi:Kigogo Wa Ikulu Adaiwa Kutumia Fedha za Umma ( Laki 8 ) Kufanya Masaji

Monday, December 21, 2015


Harakati za kuwasaka wabadhirifu wa fedha za umma ili waingie kwenye msululu wa opareshini ya kutumbua majipu iliyoanzishwa na serikali ya awamu ya tano zimeibua tuhuma nyingine zinzomhusu moja kati ya vigogo anayeiwa kuwa mfanyakazi wa Ikulu.

Taarifa zilizochapishwa katika gazeti la MwanaHalisi zinaeleza kuwa uchunguzi uliofanywa na gazeti hilo umebaini nyaraka zinazoonesha kigogo huyo alitumia fedha za walipa kodi kiasi cha shilingi 821,997.24 kwa ajili ya kufanyiwa huduma ya kukandwa mwili (massage), katika hotel ya kifahari ya Four Seasons Safari Lodge iliyoko ndani ya mbuga za wanyama za serengeti, Arusha.

Kwa mujibu wa gazeti hilo, stakabadhi waliyoipata katika hotel hiyo ilionesha kuwa kigogo huyo alifika hotelini hapo April 17 mwaka huu tarehe ambazo Rais mstaafu Jakaya Kikwete alikuwa na ziara jijini Arusha.

Imeelezwa kuwa kigogo huyo ambaye hotel hiyo haikutaka kumtaja jina alilala katika chumba namba 9017 na alikuwa na mrembo wake ambaye kwa pamoja walipata huduma zilizoingizwa kwenye stakabadhi iliyolipiwa na Ikulu.

Mbali na huduma ya Massage, huduma nyingine zilizoorodheshwa nakala ya ankara hiyo ni usafi wa nguo ambao uligharimu shilingi 676,000.

Katika kutafuta kujiridhisha, gazeti hilo lilimpigia simu afisa wa hotel ya Four Seasons Safari Lodge ambaye licha ya kukataa kutoa maelezo alikiri kuwapokea baadhi ya wafanyakazi wa Ikulu katika siku tajwa.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU