ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

Aliyekuwa Mkurugenzi wa TAKUKURU, Dr Edward Hosea, Kutema Cheche

Saturday, December 19, 2015



Aliyekuwa Mkurugenzi wa TAKUKURU, Dr Edward Hosea, anatarajiwa kutapika cheche wakati wowote kuanzia sasa kwa lengo la kutumbua majipu ya vigogo wa serikali na makada waliokuwa wakimfunga mikono na miguu wakimzuia kufanya kazi yake kwa ufasaha na umakini unaotakiwa.

Katika cheche zake hizo, mtaalamu huyo wa masuala ya rushwa na ufisadi, ataweka hadharani majina ya vigogo na makada wa chama waliokuwa wakimchimba mkwara na kuwaachia wafanye yao ili kulinda kibarua chake tukufu.

Katika orodha hiyo ya Dr Hosea wamo watu wazito kutoka serikalini waliokuwa wakimuandikia vimemo mara kwa mara wakati wanapopitisha makontena yao bila kulipia ushuru na kuikosesha serikali mabilioni ya shilingi za mapato.

Aidha, inasakikiwa kwamba kwenye orodha pia wamo wauza unga na majangili wakubwa waliokuwa wakipitisha unga na vipusa mtawalia, kupitia banadari ya Dar es Salaam bila kuguswa na mtu yeyote. Pia wamo vigogo waliomshika mikono wakati anashugulikia skandali ya EPA, ESCROW na nyinginezo.

Mtakumbuka kwamba kuna kada mmoja wa ngazi ya juu anayetajwatajwa sana kuhusika katika biashara haramu ya meno ya tembo ambaye meno hayo yalipatikana yamepakiwa kwenye meli yake siku za nyuma yakiwa yamesafirishwa hadi nchi za mbali.

MAONI YANGU
Magufuli jiandae kwenda mbali zaidi kushughulikia waliotoa vimemo, kwa muktadha huo utakuwa umeiteketeza CCM nzima kuanzia juu mpaka chini.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU