ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

BONDIA FRANCIS CHEKA (SMG) NAMNA ALIVYOTOA NAFASI YA KUPIGWA NA BONDIA THOMAS MASHALI SIKUKUU YA KRISMASI UWANJA WA JAMHURI MOROGORO 2015.

Monday, December 28, 2015

Francis Cheka kushoto na Thomas Mashali kulia. Juma Mtanda, Morogoro. Bingwa wa ngumi za kulipwa Tanzania, Francis Cheka (SMG) amesherehekea vibaya sikukuu ya krismasi baada ya kukung’utwa kwa pointi na bondia Thamas Mashali katika pambano...\
Francis Cheka kushoto na Thomas Mashali kulia.

Juma Mtanda, Morogoro. 
Bingwa wa ngumi za kulipwa Tanzania, Francis Cheka (SMG) amesherehekea vibaya sikukuu ya krismasi baada ya kukung’utwa kwa pointi na bondia Thamas Mashali katika pambano lisilo la ubingwa la raundi 10 uzani wa kg 77 lililofanyika kwenye uwanja wa jamhuri Desemba 25 mkoani Morogoro. 

Faraja pekee kwa Cheka katika pambano hilo ni kuondoka na kitita taslimu cha zawadi cha dola 700 na mdhamini wake Chief Ndamile Mtinginya aliyeahidi kutoa dola 1000 endapo angeshinda pambano na kujikuta ikimegwa na Thamas Mashali aliyepata dola 300 baada ya kumshinda.
Mashali aliweza kushinda pambano hilo dhidi ya Cheka kwa pointi zilizotolewa na majai baada ya pambano kumalizika. 

Jaji namba moja Hamisi Kimanga alimpa, Mashali pointi 94 dhidi ya Cheka 96 wakati jaji namba mbili, Kulwa Makalanga alimpa, Cheka pointi 93 dhidi ya, Mashali 96 na jaji namba tatu, Pasala Chaulembo alitoa pointi 93 kwa, Cheka huku Mashali akipata pointi 97. 

Kutokana na poiniti hizo Mwamuzi wa pambano hilo, Ally Bakari Champion alimtangaza bondia, Thomas Mashali kuwa bingwa. 

Dalili za ushindi kwa Mashali zilizjitokeza mapesa hasa katika raundi ya tatu kufuatia kumsukumia konge zito Francis Cheka aliyeyumba na kuendeleza kumimina ngumi mfululizo zilizomlazimu mpinzani wake ajihami kwa kuziba uso. 

Raundi ya nne bondia Francis Cheka aliweza kujibu mapigo kwa kurusha Makonde yaliyomfanya Thomas Mashali naye aige mbinu ya kuficha uso katika raundi nyingine wakishambuliana kwa zamu. 

Katika raundi ya 10 mabondia hao walicharuka kwa kuongeza umakini mkubwa kwa kurusha ngumi zenye malengo kabla ya kengele ya kuashiria kumalizika kwa mchezo huo uliojaza mamia ya mashabiki wa ngumi.


Francis Cheka kushoto na Thomas Mashali kulia. 

Pambano hilo lilitanguliwa na michezo ya utangulizi kwa mchezo kati ya bondia Deo Njiku wa Morogoro na Vichent Mbilinyi wa Dar es Salaam la raundi sita uzani wa kg 63 ambapo Deo Njiku alipoteza pambano kwa TKO raundi ya pili. 

Njiku alishindwa kuendelea na mchezo baada ya kukung’utwa ngumi nzito na Mbilinyi iliyomchana juu ya jicho na mwamuzi, Kulwa Makalanga kuamuru pambano hilo kumalizika kwa TKO.. 

Katika pambano lingine la utangulizi la raundi sita kg60 bondia Mohamed Matumla wa Dar es Salaam alishinda pambano mbele ya Kudra Tamimu wa Morogoro kwa pointi 97, 98, 95 dhidi ya mpinzani wake Tamimu aliyepata pointi 54, 55 na 54. 

Bondia Mfaume Mfaume wa Dar es Salaam alifanikiwa kumnyamazisha bondia Osama Kaogwa wa Morogoro kwa kumpiga TKO raundi ya kwanza katika uzani wa kg 60 huku pambano la ubingwa kati ya wanadada Lulu Kayage kg50 na Mwanne Haji kg 49, Kayage alifanikiwa kutwaa ubingwa wa TBPC kwa ushindi wa pointi. 

Ushindi huo kwa Kayage alipata baada ya kupata pointi 97,98 na 95 wakati mpinzani wake akipata pointi 93,93,96 wakati Omari Matenga akipata ushindi wa pointi 39, 39 mbele ya Sadik Stolo aliyepata pointi 39, 38 katika pambano la kg 64 la raundi nne. 

Bondia Alex Peter wa Dar es Salaam ndiye aliyeanza pamzia la TKO kufuatia kumtandika mpinzani wak George Marthin wa Morogoro katika raundi ya tatu kati ya raundi nne za mchezo huo.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU