ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

TANZANIA KURUDISHIWA KIASI KIKUBWA CHA PESA KUTOKA STANBIC BANK

Tuesday, December 1, 2015

Tanzania kurudishiwa dola za kimarekani milioni 6 kutoka stanbic Tanzania kupitia kampuni ya EGMA
Tanzania inatarajia kurudishiwa dola za kimarekani milioni sita sawa na shilingi za kitanzania bilioni 14 zilizotozwa isivyostahili na benki ya Stanbic Tanzania kupitia kampuni ya EGMA.
Fedha hizo zinarejeshwa kwa Tanzania baada ya benki ya Stanbic Tanzania kupitia kampuni ya EGMA kuongeza asilimia moja ya riba baada ya serikali kukopa dola milioni mia sita kwa ajili ya kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo mwaka 2012 na 2013 na kutakiwa kuzilipa katika kipindi cha miaka 7 kwa riba ya aslimia 1 nukta nne na badala yake ikatozwa asilimia mbili nukta nne ya mkopo wote hali iliyotokana na benki kuu kubaini baadhi ya matatizo.
 
Kwa mujibu wa Balozi Ombeni Sefue udanganyifu wa utaratibu wa kumtafuta wakala wa ndani yaani Local Agent uliofanywa na benki ya Stanbic Tanzania ulibainika kutokana na uchunguzi uliofanywa na kampuni ya Serious Fraud Office ya London na kufungua kesi ambayo kampuni hiyo ilipata ushindi November 30, 2015 na kuiwezesha Tanzania kurejeshwa fedha hizo huku Balozi Sefue akieleza hatua zinazochukuliwa ndani ya Tanzania kuhusiana na kampuni ya EGMA na benki ya Stanbic Tanzania.
 
Aidha Balozi Sefue ameishukuru serikali ya uingereza kwa ushirikiano na kuyataka mataifa mengine ya Ulaya kuzisaidia nchi zinazoendelea kupambana na rushwa kutokana na ulaghai unaofanywa na makampuni ya nchi za ulaya badala ya kuzinyooshea vidole kuwa zimeshindwa kupambana na rushwa.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU