ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

Tido Mhando akutwa na kesi ya kujibu

Monday, August 27, 2018

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemkuta na kesi ya kujibu aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa zamani wa (TBC) Tido Mhando katika kesi yake ya matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia serikali hasara ya Sh.Mil 887.1 ambapo ataanza kujitetea September 20 2018.

Uamuzi huo umetolewa na Hakimu Mkazi Mkuu Huruma Shaidi baada ya Mwendesha Mashtaka wa Takukuru, Leornad Swai kufunga ushahidi wa mashahidi 5 wa upande wa mashtaka.

Hakimu Shaidi amesema amepitia ushahidi wote wa mashahidi watano ulioletwa na upande wa mashtaka na kuona mshtakiwa ana kesi ya kujibu, ambapo ameahirisha kesi hadi September 20 2018 ili Tido aanze kujitetea.

Katika kesi hiyo Tido anakabiliwa na mashtaka manne ya kutumia madaraka vibaya na moja la kuisababishia Serikali hasara ya Sh.Milioni 887.1 na miongoni mwa mashahidi  wa upande wa mashtaka waliotoa ushahidi ni Ofisa uchunguzi wa Takukuru Victor Lesuya Mwanasheria wa TBC  Gwakisa Mlawa na Mkurugenzi Mkuu mstaafu wa TBC Clement Mshana.

Katika kesi hiyo inadaiwa kuwa June 16, 2008 Mbando akiwa Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Tido ambaye alikuwa mkurugenzi wa TBC  kwa makusudi alitumia madaraka yake vibaya kwa kusaini mkataba wa kuendesha na utangazaji wa vipindi vya televisheni kati ya TBC na Channel 2 Group Corporation (BV1) bila ya kupitisha zabuni, kitu ambacho ni kinyume na Sheria ya Manunuzi na kuinufaisha BVl.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU