ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

Waziri wa Habari Sanaa na Michezo Harrison Mwakyembe Aomboleza Kifo cha Mzee Majuto

Thursday, August 9, 2018

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison G. Mwakyembe (Mb) amesema Serikali imepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha msanii nguli wa filamu nchini Bw. Amri Athumani  maarufu kama King Majuto  kilichotokea jana usiku katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dar es Salaam. 

Aidha, Dkt. Mwakyembe amepokea salamu za rambirambi kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kuondokewa na msanii huyo mkongwe katika tasnia ya filamu nchini.

 Waziri Mwakyembe amemshukuru sana Mhe. Rais kwa ukaribu alionao na wanasanaa kwa ujumla wao na kwa kufuatilia kwa karibu matibabu ya King Majuto ndani na nje ya nchi. 
 
"Serikali imekuwa ikishirikiana kwa ukaribu na familia ya King Majuto tangu wakati wa kumuuguza na kumpeleka nchini India kupata matibabu zaidi. Tutaendelea kuwa karibu na familia yake katika kipindi hiki kigumu cha msiba", amesisitiza Dkt.Mwakyembe. 
 
Marehemu King Majuto alianza kazi ya uigizaji zaidi ya miongo minne iliyopita hadi anafikwa na mauti King Majuto alikuwa akiendelea na kazi yake katika tasnia ya filamu. 
 
Dkt. Mwakyembe ametoa pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki, Rais wa Shirikisho la Filamu, Chama cha Wasanii wa Filamu, wanasanaa, wadau na wapenzi wote wa filamu nchini kwa kuondokewa na mpendwa wao mzee King Majuto. 

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU