ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

UFISADI WAMWEKA MAMA SULUHU MATATANI

Wednesday, April 6, 2016


KAMATI ya Bunge ya Katiba na Sheria, imeagiza kufanyika uchunguzi haraka katika jengo la ofisi ya Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan ili kuweza kubaini ubadhirifu uliofanywa na wataalamu waliohusika katika mchakato wa ujenzi wa jengo hilo.

Akizungumza jana na waandishi wa habari Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mohamed Mchengerwa ambaye pia ni Mbunge wa Rufiji alisema hatua hiyo imefikiwa baada ya kamati hiyo kufanya ukaguzi katika jengo hilo na kubaini limejengwa chini ya kiwango.
“Tumetembelea jengo hilo na kujionea limetumia fedha nyingi lakini limejengwa chini ya kiwango kwani halina hata miaka tisa lakini lina ufa mkubwa ambao unahatarisha maisha ya wafanyakazi ndani ya jengo hilo,” alisema Mchengerwa.

Alisema jengo hilo limetumia zaidi ya Sh bilioni 8 katika ujenzi, lakini limejengwa chini ya kiwango.

Aliongeza kuwa kisheria fedha zilizopangwa kwa ajili ya mradi huo zilitakiwa zibaki asilimia 20 kwa ajili ya ukarabati lakini zimebaki Sh milioni 200 tu na hakuna maelezo ya kujitosheleza.

Mchengerwa alisema hali hiyo imesababisha kamati hiyo kuagiza uchunguzi ufanyike na wataalamu waliohusika wachukuliwe hatua za kisheria kwa kufunguliwa kesi za jinai na madai.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU