ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

DWIGHT YORKE AJIPIGIA DEBE UMENEJA ASTON VILLA, ADAI ANA SAPOTI YA SIR ALEX FERGUSON!!

Thursday, April 7, 2016

DWIGHT-YORKE

Dwight Yorke ameishauri Bodi ya Aston Villa kumpa Nafasi iliyo wazi ya Meneja wa Klabu hiyo.
Villa sasa wanasaka Meneja wao wa 3 Msimu huu baada ya Remi Garde kuachia ngazi Wiki iliyopita.
Garde, ambae alimbadili Tim Sherwood Mwezi Novemba hapo Villa, ameonekana kuwa chaguo bovu baada ya kushinda Mechi 2 kati ya 20 za BPL, Ligi Kuu England.
Hivi sasa Villa wapo mkiani mwa BPL na kupona kwao wasishuke Daraja itakuwa ni miujiza mikubwa.
Lakini Dwight Yorke, alieichezea Villa kati ya 1989 na 1998 na kuifungia Bao 97 katika Mechi 292 kabla kuhamia Man United, amesisitiza yeye anaweza kuwa na mafanikio makubwa akipewa fursa ya kuiongoza Klabu hiyo.
Akiongea, Yorke, ambae alikuwa na mafanikio makubwa akiwa Mchezaji wa Man United, ameeleza: “Wamejaribu uzoefu, wamejaribu Mameneja wasiojulikana na hawajapatia. Nahisi watatafuta Mtu mzoefu lakini wakati mwingine unahitaji Mtu anaeijua Klabu ya Soka na ambae ataleta uchangamfu kwenye Klabu!”
Yorke aliongeza: “Watu hawajui nimetwaa Ubingwa wa Daraja la chini Championship. Hiyo ilikuwa mara pekee nilipocheza nje ya Ligi Kuu England nikiwa na Sunderland kwenye Championship. Hivyo naijua Ligi hiyo kama Mchezaji. Nawafahamu Wachezaji wa Villa na utamaduni wote wa Klabu hiyo!”
Yorke amesisitiza: “Nitaiomba kazi hii ya Meneja wa Villa na natumai watanipa nafasi ya usaili. Nina uzoefi mkubwa na nilicheza chini ya Mameneja Bora na nimeongea na Sir Alex Ferguson ambae amenipa sapoti kwa kazi hii! Naamini naiweza na wanipe tu nafasi ya usaili!”
LIGI KUU ENGLAND
Ratiba:
Jumamosi Aprili 9
1445 West Ham v Arsenal 
1700 Aston Villa v Bournemouth  
1700 Crystal Palace v Norwich              
1700 Southampton v Newcastle            
1700 Swansea v Chelsea   
1700 Watford v Everton    
2030 Man City v West Brom        
Jumapili Aprili 10
1530 Sunderland v Leicester                 
1800 Liverpool v Stoke               
1800 Tottenham v Man United              
Jumatano Aprili 13
2200 Crystal Palace v Everton          

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU