ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

BAADA YA KUIONA YANGA JUZI,KOCHA WA AL AHLY ANENA HAYA...!!

Monday, April 11, 2016



KOCHA wa timu ya soka ya Al Ahly, Martin Jol, amesema uimara wa safu ya ulinzi ya Yanga ilikuwa kikwazo kibwa kwao wasiibuke na ushindi juzi. Timu hizo ziliumana katika mchezo wa kwanza Raundi ya Pili Ligi ya Mabingwa Afrika na kumalizika kwa sare ya bao 1-1 katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Al Ahly walitangulia kupata bao la mapema mfungaji akiwa Amri Gamal dakika ya 11 kabla ya Yanga kusawazisha dakika ya 18 baada ya beki wa Ahly, Ahmed Hegazy kujifunga katika harakati za kuokoa.
Akizungumza baada ya mchezo huo, Jol alisema ulikuwa mzuri vijana wake walicheza vizuri na kutengeneza nafasi nyingi za mabao, lakini kikwazo ilikuwa ni umaliziaji baada ya kazi nzuri ya mabeki wa Yanga.
“Mchezo ulikuwa mzuri na mgumu ingawa safu ya ulinzi ilifanya kazi nzuri kwa upande wa wenyeji, lakini kwa ujumla mchezo ulikuwa mzuri. Yanga ni timu inayocheza mpira mzuri wenye pasi nyingi na hii inatulazimu katika mchezo wa marudiano kutumia mipira mirefu ili tuweze kupata ushindi hata wa mabao 2-0, “ alisema Jol.
Kwa upande wake, kocha wa Yanga Hans Pluijm, alisema mchezo ulikuwa mgumu kwa sababu walikutana na timu bora Afrika ambayo inaundwa na wachezaji wenye uzoefu na vipaji vya hali ya juu.
Alisema ameona upungufu wa wapinzani wao na wanajipanga kwa ajili ya mchezo wa marudiano nchini Misri na kuahidi watajitahidi kupambana ili kupata bao la ugenini kama walivyofanya wapinzani Al Ahly.
“Nawapongeza vijana wangu walijitahidi kupambana, lakini bahati haikuwa kwetu ingawa tulicheza na timu bora Afrika yenye wachezaji wanye vipaji vya hali ya juu katika kuuchezea mpira.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU