ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

NDEGE ZAGONGANA UWANJA WA NDEGE INDONESIA

Tuesday, April 5, 2016



Uwanja wa ndege wa mji wa Jakarta nchini Indonesia umefungwa kwa muda baada ya ndege mbili kugongana.
Ndege ya kubeba abiria ya shirika la Batik Air ilikuwa ikipaa ubawa wake ulipogonga sehemu ya nyuma ya ndege ya shirika la TransNusa iliyokuwa ikibururwa kwenye njia ya kutumiwa na ndege kupaa au kutua.
Ubawa wa ndege hiyo iliyokuwa ikipaa uliwaka moto.
Maafisa wanasema hakuna aliyejeruhiwa wakati wa ajali hiyo iliyotokea Jumatatu usiku.
Abiria wote waliondolewa salama.
Kisa hicho kilitokea katika uwanja wa ndege wa Halim Perdanakusuma mjini Jakarta ambao sana hutumiwa kwa safari za ndege za ndani ya nchi.
Kwa mujibu wa shirika la habari la AFP, ndege hiyo ya Batik Air ilikuwa na watu 49, abiria pamoja na marubani.
Msemaji wa kampuni ya Lion Air Group, inayomiliki Batik Air ameambia mashirika ya habari ya kimataifa kwamba rubani amekatiza safari baada ya ajali hiyo na abiria wako salama.
Ndege
Maafisa wa wizara ya uchukuzi ya Indonesia wamesema ndege hizo ziliharibiwa wakati wa kisa hicho. Video iliyopakiwa mtandaoni inaonesha miali ya moto ikitoka kwenye ubawa wa ndege ya Batik Air.
Indonesia ina historia mbaya ya usalama wa ndege licha ya kuendelea kufana na uchukuzi wa ndege hasa ndege za kubeba abiria za bei nafuu.
Mwaka 2013, ndege ya Lion Air ilipita njia ya uwanja wa ndege wa Denpasar, Bali na kutumbukia baharini. Watu 22 walijeruhiwa.
Mwaka uo huo, ndege nyingine ya Lion Air iliteleza ikitua kisiwa cha Sulawesi na kugonga ng’ombe.
Mwaka 2014, ndege ya kampuni ya AirAsia nchini Indonesia iliyokuwa safarini kutoka Surabaya hadi Singapore ilianguka baharini na kuua watu wote 162 waliokuwa ndani.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU