ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

Mzaha wa Google Siku ya Wajinga waleta balaa

Friday, April 1, 2016

Google

Google imelazimika kuondoa kitufe cha Siku ya Wajinga kutoka kwenye huduma yake ya barua pepe ya Gmail baada ya watu wengi kulalamika.
Kitufe hicho kilikuwa kinatuma video za mzaha kwa watu walio kwenye anwani ya mtu.
Kitufe hicho kilikuwa kimewekwa karibu na kitufe cha kawaida cha kutuma barua pepe na kiliwawezesha watumizi wa Gmail kusitisha mawasiliano ya kawaida na badala yake kutuma video fupi ya gif ya kibonzo kikiweka chini maikrofoni.
Watu wengi wamelalamika sana kuhusu kitufe hicho kwenye kumbi za Google.
Kuna wanaosema wamefutwa kazi baada ya kuwatumia wakubwa wao barua pepe za mzaha, wengine wanasema wametuma barua pepe za mzaha kwa kampuni ambazo walikuwa wanaomba kazi.
Mwandishi mmoja aliandika kwamba alikuwa anataka kutuma makala zake kwa mhariri na muda ulikuwa unapita akatuma haraka. Alisubiri jibu lakini hakupata. Baadaye aligundua kwamba kimakosa alibofya kitufe cha mzaha.
Kampuni hiyo imeondoa kitufe hicho na kuomba radhi.
"Inaonekana kana kwamba tumejitania sisi wenyewe mwaka huu,” Google imesema kupitia taarifa.
"Kutokana na hitilafu katika utengenezaji wa kitufe hiki, kiungo cha kuweka maikrofoni chini (MicDrop) kilisababisha kilio kuliko kicheko. Tunaomba radhi.”
Google ilitangaza kuanzishwa kwa Gmail tarehe 1 Aprili 2004 na wakati huo wengi walidhani ulikuwa mzaha wa Siku ya Wajinga.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU