ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

CHADEMA, ACT Wazalendo Wasusia Uchaguzi wa Marudio Tanga

Sunday, August 26, 2018

Vyama vya CHADEMA, ACT Wazalendo na NCCR Mageuzi vimetangaza kugomea kushiriki uchaguzi wa udiwani katika Kata ya Mwanzage jijini Tanga kwa kile walichoeleza ni kuwepo kwa zuio la mahakama juu ya uchaguzi huo.

Wakiongea katika mkutano wa pamoja, viongozi hao wamesema mbali na zuio la mahakama lakini hawaoni kama uchaguzi utakuwa wa huru na haki kutokana na kuwepo kwa mazingira yasiyoridhisha ikiwemo ucheleweshwaji wa kuchukua fomu za kugombea.

''Sababu mama ni zuio la mahakama linaloonesha kufanya uchaguzi ni batili, pili katika uchaguzi uliofanyika kata ya Mabokweni haukuwa wa haki pamoja na matumizi makubwa ya nguvu ya dola', amesema Katibu mkuu wa CHADEMA wilaya ya Tanga Jonathan Baweji.

Naye Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Hamin Kidege ametaja sababu ya chama chao kutoshiriki ni kukosekana kwa uungwana 'Fair play' katika chaguzi za kata mbalimbali zilizopita hivyo hawaoni kama katika kata hii mambo yamebadilika.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi wilaya ya Tanga, Richard Abel amesema chama chake kimeamua kuungana na vyama vingine kujitoa katika uchaguzi huo, kutokana na kupuuzwa kwa agizo la mahakama la kutofanyika kwa uchaguzi huo.

Kwa mujibu wa ratiba ya Tume ya taifa ya uchaguzi (NEC), uchaguzi wa udiwani na wambunge katika kata na majimbo yaliyotangazwa utafanyika Septemba 16, mwaka huu.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU