ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

Waarabu wa Yanga wamnasa ‘Kamusoko’

Saturday, July 9, 2016

NA Erick Pekepeke
KIKOSI cha Mo Bejaia cha nchini Algeria kilichoifunga Yanga bao 1-0 katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika, kimezidi kujiimarisha baada ya kusajili kiungo matata kutoka Ufaransa mwenye uwezo mkubwa ndani ya dimba kama ilivyo kwa Thaban Kamusoko na huenda akawepo mchezo wa marudiano Uwanja wa Taifa.
Waarabu hao wamemsajili, Youcef Touati, kutoka katika klabu ya
Champly inayoshiriki Ligi Daraja la Tatu nchini Ufaransa kwa mkataba wa miaka mitatu kuwasaidia katika michuano mbalimbali ikiwamo ya kimataifa.
Kiungo huyo ambaye ana umri wa miaka 27, amezaliwa katika kitongoji cha Saint Denis nchini Ufaransa akichezea timu mbalimbali nchini humo na sasa anahamishia makali yake katika klabu hiyo ya Mo Bejaia.
Kiungo huyo ni mkali wa kupiga pasi za mwisho na pia ni mzuri linapokuja suala la kuzuia mashambulizi ya timu pinzani lakini pia anao uwezo mkubwa wa kufunga kama ilivyo kwa Mzimbabwe wa Yanga, Thaban Kamusoko.
Timu ambazo amepitia kiungo huyo ni Red Star ya Ligi Daraja la Tatu nchini Ufaransa ambapo aliichezea michezo 27 akifunga mabao mawili msimu wa 2011/12, kabla ya kujinga na FC Istre ya Ligi Daraja la Pili akicheza michezo 11 lakini hakufanikiwa kufunga.
Msimu wa 2013/14 alijiunga na FC Tour ya Ligi Daraja la Pili na alicheza michezo sita tu kabla ya kujiunga na Epinal ya Ligi Daraja la Tatu akifunga mabao mawili katika michezo 21 na baadaye kuhamia Champly aliyoichezea michezo 20 na kufunga mabao  matatu.
Kikosi hicho mwishoni mwa wiki ijayo kitakutana na TP Mazembe katika mfululizo wa michuano hiyo ya Kombe la Shirikisho huku ikijiandaa kuja nchini Tanzania kumenyana na Yanga mchezo wa marudiano.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU