ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

TRA :Mapato Bandarini Yameongezeka Zaidi

Wednesday, July 6, 2016

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imesema kupungua kwa mizigo bandarini kumeathiri si Tanzania pekee bali dunia nzima na kwamba kubanwa kwa mianya ya wizi kumesababisha kuongezeka kwa mapato kutoka Sh bil 458 Aprili mwaka huu kufikia Sh bil 517. 


Aidha, TRA imesema
itaanza uhakiki wa namba za utambulisho wa mlipakodi (TIN) kutokana na kuwepo watu wenye namba mbili na wasiohakiki watalazimika kudaiwa kodi na TRA. 


Akizungumza katika mkutano na wanahabari jana, Kamishna wa TRA, Alphayo Kidata alisema upungufu huo wa mizigo bandarini umezikumba pia bandari za Beira, Msumbiji, Mombasa, Kenya na kwingineko na kusababisha mapato kupungua. 


“Lakini sisi pamoja na upungufu wa mizigo bandarini makusanyo yanazidi kuongezeka kutokana na kuzibwa mianya ya kukwepa kodi, hivyo napenda kuwapongeza wafanyakazi wote wa mamlaka na kusema kwa sasa hakuna mtu anayeweza kukwepa kodi na wale waliozoea wakae katika njia kuu,” alisema Kidata. 


Kidata alisema wananchi wanatakiwa kuwaunga mkono kwani sasa kodi inaonekana katika kufanya shughuli za serikali kama kuboresha miundombinu pamoja na kutoa elimu bure. 


Alisema TRA imefikia na kuvuka lengo la makusanyo ya kodi kwa mwaka wa fedha 2015/16 kwa kukusanya Sh trilioni 13.8 sawa na asilimia 100.04 ya lengo la kukusanya Sh trilioni 13.4 iliyokuwa imepangwa na serikali. 


Kidata alisema katika kipindi cha Juni mwaka huu, TRA imekusanya Sh trilioni 1.4 sawa na asilimia 107.83 ya lengo la kukuzanya Sh trilioni 1.3 ambapo makusanyo ya mwaka wa fedha 2015/16 ni sawa na ongezeko la asilimia 23.70 la makusanyo ya mwaka 2014/15. 


Akizungumzia mashine za kielektroniki za EFDs, Kidata alisema walipoanza utoaji mashine hizo zilikuwa 5,703 na mpaka sasa mashine 1,700 zimegawiwa kwa watumiaji na wataanza kupita duka hadi duka kuhakiki matumizi ya mashine hizo. 


Kamishna wa mapato ya ndani, Elijah Mwandumbya, alisema mwaka huu wa fedha wamejipanga kuhakikisha wanaondoa changamoto kwa mtu mmoja kuwa na TIN zaidi ya moja hivyo watafanya uhakiki.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU