ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

URENO YATINGA FAINALI YA EURO 2016,YAILAZA WALES 2-0

Thursday, July 7, 2016


Ulikuwa mtanange wa kukata na shoka wa nusu fainali ya michuano ya Euro 2016 inayotimua vumbi kule nchini Ufaransa kati ya Wales iliyokuwa ikiongozwa na Gareth Bale na Ureno ikiongozwa na Christian Ronaldo.

Mtanange huo ulio kanyagwa katika dimba la Parc de Olimpique jijini Lyon, ulichezeshwa vizuri na mwamuzi Jonas Eriksson wa Sweden na mpaka mapumziko timu hizo hazikuweza kufungana ingawa kila timu ilitengeza nafasi kadhaa za kuweza kujipatia mabao laikn umaliziaji ukawa mbovu.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi zaidi na walikuwa Ureno wlianza kuhanikiza ushindi,si mwingine bali ni Christian Ronaldo kunako dakika ya 50 yaani dakika 5 tu baada ya kuanza kipindi hicho anafunga bao zuri kwa kichwa akiunganisha mpira wa kona fupi toka kwa Guerreiro.

Na dakika 3 baadaye Ronaldo anapiga shuti kali langoni mwa Wales akiwa umbali wa mita 25 na mpira huo unawapita walinzi wa Wales ambapo Luis Nani wa Ureno anaserereka na kuuunganisha wavuni akiianikia timu yake bao la pili.

Kuona jahazi linazama kocha wa Wales Chris Coleman anamtoa Joe Ladley na kumwingiza Sam Vokes huku akibadili mfumo toka 3-5-1-1 na kucheza 4-3-1-2,lakini hiyo haikusaidia kubadili matokeo mbele ya Ureno waliokuwa wakicheza mfumo wa 4-1-3-2.
Sasa Ureno anamsubiri mshindi wa mchezo wa leo kati ya wenyeji Ufaransa na Ujerumani kucheza naye fainali siku ya jumapili Julai 10 2016 katika dimba la Stade de France,Paris.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU