ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

Simba wamficha Mavugo hotelini

Saturday, July 9, 2016

Na Erick Mlelwa
WAKATI zikiwapo taarifa kuwa Vital’O ya Burundi imekamilisha usajili wake huku likiwamo jina la Laudit Mavugo, mashabiki wa Simba wanaweza wakaendelea kufurahi kwani straika huyo inasemekana amefichwa na Wekundu hao wa Msimbazi.
Taarifa kutoka Simba zinadai kuwa
straika huyo amefichwa moja ya hoteli kubwa nchini Burundi huku wakimhudumia kila kitu na muda wowote wanamleta nchini ili kumalizana naye.
Simba wamekuwa wakimfukuzia mkali huyo wa mabao tangu msimu uliopita lakini ilishindikana baada ya klabu yake ya Vital’O kumwekea ngumu na sasa Wekundu hao wa Msimbazi wanataka kufanya umafia.
Simba na Mavugo walifikia makubaliano lakini Vital’O wakaweka dau kubwa lililowashinda Wekundu hao wa Msimbazi wakaamua kurudisha majeshi nyuma ingawa sasa wanataka kufanya kweli.
Kigogo mmoja wa Simba aliliambia DIMBA Jumatano kuwa licha ya taarifa kuenea kwamba straika huyo yupo kwenye usajili wa Vital’O, mashabiki wa Wekundu hao wa Msimbazi wasiwe na wasiwasi kwani kila kitu kinakwenda vizuri.
“Ni kweli kwamba kuna taarifa za Vital’O kumjumuisha kwenye usajili wao lakini hilo lisiwape presha mashabiki wetu kwani tunafanya mipango yetu kimya kimya,” alisema kigogo huyo.
DIMBA lilikwenda mbali na kumtafuta straika huyo ili kuzungumzia maisha yake ya msimu ujao ambapo alisema yupo nchini kwao Burundi akisubiri kutumiwa tiketi na Simba aje Tanzania.
“Nilishamaliza mkataba na Vital’O na sasa nipo huru, nimefanya mazungumzo na Simba na ninachosubiri ni wao wanitumie tikieti. Ni kweli kwamba bado Vital’O wanataka kunisainisha mkataba mpya lakini siyafikia makubaliano nao,” alisema.
Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Simba, Zachari Hanspope ambaye kwa sasa yuko Marekani, amewataka mashabiki na wanachama wa Simba kutokuwa na hofu juu ya ujio wa Mavugo kwa vile mtu aliyemwachia jukumu hilo yuko makini.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU