ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

IMEVUJA;CHADEMA YAJIPANGA KUMFUKUZA LOWASSA,TUNDU LISSU AONGEA HAYA MAZITO JUU YA MCHAKATO UTAKAVYOKUWA

Thursday, January 14, 2016



Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimeibuka na kuutaka uongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), umfukuze uanachama aliyekuwa mgombea urais kupitia chama hicho, Edward Lowassa.

 Hatua hiyo ya CCM imekuja siku moja baada ya Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu, kusema ufisadi ni ajenda yao ya kudumu. Kutokana na kauli hiyo ya Lissu, CCM imetaka Chadema imfukuze Lowassa, ili kutekeleza kwa vitendo kauli ya Lissu .

 Lowassa ambaye ni Waziri Mkuu mstaafu, alihama CCM baada ya kuenguliwa kuwania urais kupitia chama hicho na kujiunga na Chadema ambako alipewa nafasi ya kugombea urais kupitia chama hicho na kuungwa mkono na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

 Aidha, CCM imeitaka Chadema kutangaza hadharani kumuunga mkono Rais Dk. John Magufuli, kwa kazi anazozifanya, ikiwamo kukemea ufisadi badala ya kuzungumza kwa maneno bila vitendo.

 Kauli hiyo, ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Katibu wa Nec, Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnaye, ambaye alisema chama hicho kimekosa ajenda kwa kuwakumbatia mafisadi.

 “Tundu Lissu nimemwelewa alichokisema lakini waache kuwahadaa Watanzania kuwa ufisadi ni ajenda yao. Wakitaka kufanya hivyo kwanza wamfukuze Lowassa na pia watangaze hadharani kumuunga mkono Rais Magufuli. Hapo tutawaelewa badala ya kuzungumza tu bila vitendo,” alisema Nape.

 Akizungumzia sababu za CCM kutomfukuza Lowassa akiwa ndani ya chama hicho, alisema jambo hilo lilifanyika kupitia kampeni yake ya vua gamba.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU