ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

WEZI WA MALI YA UMMA ! RAIS MAGUFULI KUTUMBUA MAJIPU YOTE MPAKA YAISHE

Friday, January 22, 2016

Rais John Magufuli akicheza ngoma ya kimasai pamoja na wananchi muda mfupi baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) jana, akiwa njiani kwenda Arusha kwa ziara ya kikazi. 

RAIS John Magufuli ametoa mwito kwa Watanzania kumuombea ili aendelee kuwashughulikia wote wanaofanya ubadhirifu wa fedha za umma kupitia kampeni yake ya kutumbua majipu. 

“Nataka niwahakikishieni kuwa nitaendelea kutumbua majipu yote mpaka yaishe, na naomba mniombee ili kazi hii ya kutumbua majipu ifanyike kwa mafanikio,” alisema Dk Magufuli. 

Alitoa kauli hiyo wakati alipokuwa akizungumza na wananchi katika mikoa ya Kilimanjaro na Arusha jana, alipotua kwa ziara ya kikazi ikiwa ni ya kwanza kwao tangu achaguliwe kushika wadhifa huo Novemba 5, mwaka jana. 

Dk Magufuli aliwasili mkoani Arusha, ambako kesho atatunuku Kamisheni kwa maofisa wanafunzi wa kundi la 57/15 katika Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi (TMA) Monduli mkoani hapa. 

Rais Magufuli aliwasili mjini Arusha akitokea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), alikotua kwa ndege akitokea jijini Dar es Salaam na kupokewa na mamia ya wananchi. Akiwa uwanjani hapo, Rais Magufuli aliwashukuru wananchi kwa mapokezi makubwa aliyoyapata na aliwaeleza kuwa uchaguzi umekwisha, kilichobaki ni kazi tu. 

“Nawashukuru sana ndugu wananchi kwa mapokezi haya makubwa, naomba kuwahakikishia kuwa uchaguzi umekwisha na sasa kilichobaki ni kuchapa kazi tu,” alisema Rais Magufuli. 

Akiwa njiani kutoka KIA, Rais Magufuli alisimamishwa na wananchi wa njiapanda ya KIA, Kikatiti, Usa River, Tengeru na Mount Meru mjini Arusha ambako huko kote pamoja na kusisitiza kuwa uchaguzi umekwisha na kilichobaki ni kuchapa kazi, aliwahakikishia kuwa hatawaangusha. 

Aidha, Rais Magufuli alisema tayari serikali imeanza kutoa fedha kwa ajili ya kugharimia elimu ya msingi na sekondari baada ya kufuta ada na alionya kuwa watumishi wa umma hususani wakuu wa shule watakaothubutu kufanya ubadhirifu wa fedha hizo watashughulikiwa. 

Alisema yote aliyoyaahidi kwa wananchi wa mkoa wa Arusha na Watanzania kwa ujumla, ikiwemo ujenzi wa barabara za Arusha, kulipa fidia za wananchi na kufuta ada ya shule za msingi na sekondari yanatekelezwa. 

Rais Magufuli alisisitiza kuwa serikali yake haitawabagua Watanzania kwa dini zao wala makabila yao na wala haitawabagua kwa misingi ya vyama vyao na kanda zao. Aliwataka Watanzania wote kuiweka mbele Tanzania na kushirikiana kuiendeleza.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU