ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

BREAKING NEWZZ;KWA MARA YA KWANZA LOWASSA AMPA BIG UP MAGUFULI AFUNGUNGA HAYA MAZITO

Thursday, January 14, 2016



Aliyekuwa mgombea urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa, amemtembelea Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye, katika taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Hosptitali ya Taifa Muhimbili alikolazwa.

Lowassa ambaye alifika hospitalini hapo jana saa 7:00 mchana akiwa na mke wake Regina, aliwapongeza viongozi wengine ambao wamekwisha kufika hospitalini hapo kumjulia hali Sumaye, wakiwamo Rais John Magufuli, Rais Mstaafu na Mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Lowassa alisema hilo ni jambo jema la  kiungwana, la kuheshimiana na kutendeana mema.


Wengine waliomtembelea Sumaye hospitalini hapo ni Waziri Mkuu Mstaafu, Dk. Salim Ahmed Salim na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema,  Prof. Mwesiga Baregu.

Lowassa na mkewe walifika hospitalini hapo muda mfupi baada ya Prof. Baregu na Dk. Salim kumuona Sumaye.

Akizungumza baada ya kutembelewa na hospitalini hapo, Sumaye alisema anaendelea vizuri.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa JKCI, Prof. Mohamed Janabi, alisema hali ya mgonjwa huyo imeendelea kuimarika kila siku.
 
Sumaye alilazwa katika taasisi hiyo siku sita zilizopita kwa matibabu ya moyo.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU