ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

CHAN: Tunisia yatoka sare na Nigeria

Friday, January 22, 2016

Tunisia

Mechi za mkumbo wa pili Kundi C katika michuano ya kombe la taifa bingwa Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani zimemalizika kwa klabu zote kutoshana nguvu.
Nigeria walitangulia kwa kutoka sare ya 1-1 na Tunisia mjini Kigali.
Bao la Nigeria lilitingwa wavuni na Elvis Chikatara dakika ya 51.
Tunisia walihakikisha wanaondoka na alama moja baada ya kusawazisha kupitia Ahmed Akaichi dakika ya 69. Akaichi alikuwa ametumbukiza mpira kimiani kwa kichwa dakika ya kwanza lakini alikuwa ameotea.
Kwenye mechi ya pili, Issa Moussa alifungia Niger bao la kwanza nao Guinea wakapata lao kupitia Alseny Camara.
Ammadou Issa, aliyekuwa ameingia uwanjani kama nguvu mpya, aliweka Niger kifua mbele dakika ya 49.
Aboubacar Bangoura hata hivyo alikomboa bao hilo na mambo yakasalia hivyo hadi kipenga cha mwisho kilipopulizwa.
Kwa sasa Nigeria wanaongoza kundi hilo na alama nne, Tunisia na Guinea wakifuata wakiwa na alama mbili kila mmoja, nao Niger inavuta mkia ikiwa na alama moja pekee.
Mechi za mwisho Kundi C zitachezwa Jumanne wiki ijayo ambapo Nigeria watacheza dhidi ya Guinea nao Tunisia wacheze dhidi ya Niger.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU