ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

MUZIKI WA GOSPEL TANZANIA NANI AMEULOGA?

Tuesday, March 29, 2016


Kupitia  ukurasa wake facebook Mwanaharakati Martin Bashando aliyasema maneno haya.

"Muziki wa Injili Tanzania umeanza miaka mingi sana zaidi ya Bongo fleva, lakini sijawahi kuona record ya mwanamuziki wa injili ambae amewahi kufanikiwa kifedha pamoja na kuufikisha muziki wake katika viwango ambavyo huyu mwanamuziki Diamond ameufikisha mziki wake. 

Wanamuziki wengi wa Injili wa hapo zamani walipofanikiwa katika muziki wao kidogo wengi walikimbia na kuhamia ulaya, na walipofika kule kasi ya muziki ilipungua kwao na kujikuta wanakimbizana na maisha kwa kufanya vibarua vya kufyeka garden za wazungu, kufua, kuosha sufuria, kuogesha farasi, kutunza wazee nakadharika, lakini pamoja na kuwa waliendelea na fani zao Polepole lakini hawakuweza kusimamia kipaji hadi kufikia viwango vya kuipeperusha bendera ya nchi katika viwango hivi vya Diamond.

Kwa miaka ya 2000 hadi 2015 ndipo walichipuka wanamuziki wa Injili ambao angarau walijitahidi kidogo sana katika fani zao huku wakiwa hapa hapa nyumbani na wakashika vijimilioni na kumiliki magari pamoja na kujenga nyumba na wengine kuwa na biashara pembeni, lakini bado hawajafikia kiwango cha kuwa wanamuziki wa kimataifa bali wanakuwa wanamuziki wa afrika mashariki.

Katika mchakamchaka huo anaetuokoa kidogo ni Rose Muhando ingawa juhudi zake zinapuuzwa na watu wengi wanampiga vita vikali sana kupitia mapungufu yake ya kibinadamu.

Sasa najiuliza hapa tofauti iko wapi ama tatizo liko wapi hadi waimbaji wa nyimbo za Injili wanaishia katika kiwango kidogo na wanashindwa kupenya na kufikia levo kubwa ambazo wanastahili na kujikuta kila siku wako pale pale ingawa kiuharisia wana vipaji vikubwa sana zaidi ya bongo fleva?"

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU