ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

NAIBU WAZIR MAMBO YA NJE DR SUSAN KOLIMBA AMWAGA MISAADA UWT ,WAZEE NA WALEMAVU NJOMBE

Friday, March 11, 2016

Image result for SUSAN KOLIMBA

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Dokta Susan Kolimba Ambaye Pia ni Mbunge wa Viti Maalumu CCM Mkoa wa Njombe amehitinisha ziara yake mkoani njombe kwa kufanya kikao na baraza la umoja wa wanawake  Tanzania UWT mkoani humo ambapo ameendelea kusisitiza wanawake hao kuweka nguvu katika usimamizi  miradi ya maendeleo ya umoja huo pamoja na kuanzisha miradi mipya itakayo kuza uchumi kwa haraka zikiwemo mashine za kusaga na kukoboa alizowapa

Ziara hiyo ya siku nne iliyolenga kuyafikia makundi mbalimbali wakiwemo walemavu na wazee pamoja na kutatua baadhi ya changamoto zinazo wakabili imeonekana kuwanufaisha walengwa kwa kuwa sehemu kubwa ya changamoto
zimepatiwa ufumbuzi kwa muda mfupi kama kuwapa misaada ya chakula mavazi na vifaa vya ujenzi kwaajili ya kukamilisha ukarabati wa majengo wanayioishi

DR Kolimba pia ametumia ziara hiyo  kutekeleza baadhi ya ahadi alizo ahidi kwa wananchi kipindi cha kampeni za uchaguzi  mwaka jana ambapo akiwa wilayani ludewa ametoa vifaa kwaajili ya kukarabati soko wilayani humo kufuatia maombi ya wananchi


Baadhi ya wanufaika na misaada hiyo akiwemo Katibu wa ccm wilya ya ludewa Lusiano Mbosa na diwani wa kata ya ludewa mjini bi Monica Mchilo wamesema kuwa msaada huo wa vifaa vya kukarabati soko wilayani humo utainufaisha jamii nzima huku wakionya uongozi wa soko kutumia vifaa walivyopewa kama ilivyokusudiwa

Wakizungumzia misaada iliyotolewa na mbunge huyo mteule wa viti maalumu kwa wilaya nne za mkoa wa njombe viongozi wa umoja wa wanawake Tanzania UWT akiwemo Rosemary Lwiva mwenyekiti na mjumbu wa baraza kuu taifa Bi Farida Nurdini wamesema kwa utendaji kazi mzuri alioanza nao wanaamini kuwa mkoa wa njombe utakuwa na maendeleo makubwa

Kwa upande wao baadhi ya wazee waliopatiwa misaada pamoja na wawakilishi wa vituo vya watoto wenye ulemavu katika halmashauri zilizopatiwa ziara walikuwa na haya ya kusema

misaada Yenye thamani ya zaidi ya shi lingi milion 18 imetolewa kwa wilaya zote nne kwa umoja wa wanawake Tanzania UWT Pamoja na kwa wazeena walemavu

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU