ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

MARUFUKU KULIPANA POSHO KTK KUJADILI MATATIZO YA WANANCHI NJOMBE.....Dkt Rehema Nchimbi

Wednesday, March 2, 2016


Waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Nchini Tanzania Bi,Jenister Mhagama

Waziri Jenister Mgahama  katika mkutano na wajasiriamali mjini Njombe

Mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi ya mkoa wa Njombe ambayepia ni Mkuu wa Mkoa huo Dkt Rehema Nchimbi amesema ni marufuku kwa watumishi katika halmashauri kulipana posho katika vikao vya kujadfili matatizo ya wananchi.

kauli hiyo ameitoa leo katika kikao na wajasiriamali wadogo wadogo mjini Njombe wakiwemo mama lishe,vikoba,madereva boda boda ambapo pia pamoja na mambo mengine ametoa siku 7 kuanzia jumatano ya leo mpaka wiki ijayo kuwa tayari halmashauri zote zimeunda kamati za kushughulikia  masuala ya ajira kwa vijana.
 
 Naye Waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Nchini Tanzania Bi, Jenista Mgahama ameziagiza halmashauri zote mkoani Njombe kuhakikisha zinateua wataalamu wa kusimamia uwezeshawaji wa ajira kwa vijana katika halamshauri zote.

 Baada ya uteuzi huo amesema baraza la uwezeshai ajira taifa kwa wananchi kuanzia mwezi wa 3 mwaka huu litapita kutoa mafunzo kwa viongozi hao watakaoteuliwa.

Akiwa mjini Njombe Mh,Mgahama amesema sasa ni wakati wa kila mwananchi kumiliki uchumi wake mwenyewe na kuachana na mambo ya kumfanyia kazi mtu mwingine huku wenyewe maisha yao yakiendelea kuwa duni.

Anasema kundi la boda boda ni wakati wa kupewa kipaumbele na kuachana na kendesha boda boda ambazo siyo mali zao ambapo pia pamoja na mambo mengine aiagiza serikali mkoani Njombe kuona namna nzuri ya kulisaidia kundi hili ili liweze kujiinua kiuchumi.

Baada ya agizo hilo akasimama mwenyekiti wa boda boda mkoa Njombe ambaye anasema kuna zaidi ya madereva boda boda 600 lakini wanaomiliki boda boda zao hata 30 hawafikii jambo ambalo wanasimama kuomba msaada zaidi kupitia katika vyama vya ushirika ili viwasaidie kupewa mikopo yenye riba nafuu.

Baada ya agizo hilo la Mheshimiwa waziri naye mkuu wa mkoa wa Njombe Dkt Rehema Nchimbi ametoa siku 7 kwa halmashauri zote mkoani Njombe kuwa tayari zimeunda mabaraza hayo ya kushugulikia masuala ya ajira kwa vijana na wananchi kwa ujumla kuwasilisha ofisini kwake.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU