ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

Habari kamili. Mwanafunzi wa shule ya sekondari Mbogamo Njombe amepigwa na walimu wake mpaka kupoteza fahamu

Wednesday, October 12, 2016



Na Erick Mlelwa,Njombe
Siku chache baada ya kuripotiwa taarifa za mwanafunzi kushambuliwa kupigwa na walimu katika shule ya Mbeya day jijini Mbeya tukio la aina hiyo limemkuta mwanafunzi mwingine wa shule ya sekondari ya Mbogamo ya mjini Njombe ambaye ameshambuliwa kwa kupigwa mpaka kupoteza fahamu na
kulazwa katika hospitali ya mkoa huo na walimu 6 akiwemo mkuu wa shule hiyo Bi Helmina Mgaya.

Mwanafunzi huyo Elizabert Simfukwe wa kidato cha nne anaye kadiriwa kuwa na umri wa miaka 19 anadaiwa kufanyiwa kitendo hicho cha kikatili tangu Octoba 6 mwaka huu ambapo adhabu hiyo ameipata baada ya kukutwa na simu ya mkononi katika begi lake kinyume na sheria za shule.

Kwa mujibu wa diwani wa kata ya Ramadhani George Sanga ambako shule hiyo ipo amesema kuwa walimu hao walifikia hatua ya kumfanyia hivyo mwanafunzi wakimtaka aeleze matumizi ya simu hiyo.

Kumekuwa na usiri mkubwa kwa mamlaka za serikali kutoa ushirikiano kwa wandishi wa habari juu ya tukio hili likiwemo jeshi la polisi na idara ya elimu ambapo hata uongozo wa hospitali ya mkoa wa njombe kibena unaeleza kuwa umezuiliwa kutoa taarifa hizo na utawala wa ngazi za juu.

Lakini hata hivyo mkuu wa wilaya ya Njombe Bi Ruth Msafiri ambaye yuko nje ya wilaya kikazi amekiri kwa kwa njia ya siku kuwa na tarifa za shambulio hilo ameagiza walimu waliohusika kuendelea kushikiwa na jeshi la polisi mpaka sheria ichukue mkondo wake

Chanzo: ITV

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU