ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

SIKU YA MTOTO WA KIKE: TUJIFUNZE KUTOKA KATIKA KISA CHA MAYA

Tuesday, October 11, 2016



Katika kusheherekea siku ya mtoto wa kike kimataifa, ninawaletea kisa kifupi chenye mafunzo muhimu kwa wasichana wote duniani, kisa hichi ni cha MAYA.
Maya ni binti wa miaka 12 aishie na wadogo zake wawili wa kiume katika familia maskini. “Ndoto” yake ni kuwa mwalimu ili kuisaidia jamii yake. Umasikini wa familia yake wamfanya Maya kukaa nyumbani na wadogo zake kwenda shule. 

Ndoto yake imevunjika. Maya hana elimu wala ajira (takwimu zaonyesha 1/3 ya wanawake Tanzania hawajasoma).
Maya anajihatarisha kupata maambukizi ya VVU/UKIMWI (huku asilimia 40 tu ya wasichana umri kati ya 15-19 wakiwa na elimu juu ya ugonjwa huu) au mimba ya utotoni kwa kujiuza ilia apate chakula, hifadhi na ulinzi. Anapata uja uzito akiwa na miaka 16 (huku ¼ ya wasichana kuaniza umri wa miaka 15 ni wazazi watoto). Anajifungua kwa matatizo mtoto Maryam ambapo anaamua kubadili msimamo wa maisha yake.
Maya anajihusisha na kazi za kuajiriwa na biashara ndogo, anafanikiwa kufungua mgahawa. Sasa anaweza kumpeleka Maryam shule. 
Maryam anasoma kwa bidii na kupata udhamini wa kwenda chuo ambapo anafanikiwa kuhitimu kama Mwalimu. Mustakabali wake sasa uko mikononi mwake tofauti na ule wa Maya, na sasa Maryam anaweza kusaidia jamii yake, ndoto ambayo alikuwa nayo mama yake.
Kumbuka: Ukimuelimisha mwanaume unamueleimisha mtu mmoja, ukimuelimisha mwanamke basi unalielimisha Taifa!

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU