ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

BREAKING NEWS:HAKUNA ALIETEGEMEA KUONA TUKIO HILI MKURUGENZI AMGOMEA WAZIRI MKUU NI BAADA YA KUPEWA MAAGIZO HAYA..

Thursday, October 20, 2016

AGIZO la Waziri Mkuu Majaliwa Kassim, kuwataka watendaji wa Serikali kutoa taarifa katika vyombo vya habari juu ya mipango ya maendeleo inayofanywa na serikali, limepuuzwa na Godwin Kunambi, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma, anaandika Dany Tibason.

Leo baada ya kumalizika kwa zoezi la usafi uliofanyika ili kuadhimisha siku ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere, muasisi wa Taifa la Tanzania, Kunambi amekataa kuzungumzia lolote juu ya utekelezaji wa agizo la Waziri Mkuu la kuondoa nyumba za tope katikati ya Mji wa Dodoma.
“Siwezi kuongea jambo lolote kwa sasa ninawaachia Mkuu wa Wilaya na Mkuu wa Mkoa waongee. Bora ningekuwa nazungumza na radio au TV lakini katika gazeti siwezi kuzungumza chochote, niache tu,” amesema Kunambi alipozungumza na mwandishi wa MwanaHALISI online.

Pamoja na mwandishi kumkumbusha kuwa Mkurugenzi ndiye mtendaji mkuu wa manispaa hivyo ni vyema akatoa ufafanuzi juu ya hatua gani ambazo manispaa yake imezichukua mpaka sasa ili kutekeleza agizo la Waziri Mkuu la kuondoa nyumba za tope na kuboresha miundombinu lakini Kunambi aligoma.

Hivi karibuni baada ya kuanza utekelezaji wa kuifanya Dodoma kuwa makao makuu ya nchi, Waziri Mkuu Majaliwa alijitambulisha kwa waandishi wa habari wa Mkoa wa Dodoma na kuwaagiza wakuu wa Idara mbalimbali pamoja na watendaji wa serikali kuhakikisha wanatoa ushirikiano kwa vyombo vya habari.

“Toeni taarifa za utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya serikali katika vyombo vya habari bila kukibagua chombo chochote,” alisema Waziri Mkuu Majaliwa.

Kitendo cha Kunambi kukataa kuzungumzia mipango ya maendeleo hususani utekelezaji wa agizo la Waziri Mkuu la kuondoa nyumba za tope katikati ya mji ni kupuuza agizo lake la awali la kutaka taarifa muhimu za mipango ya maendeleo zitolewa katika vyombo vya habari bila kuvibagua vyombo hivyo.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU