ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

Nchi 10 kati ya 14 za Ulaya zasitisha msaada wa kibajeti kwa Tanzania

Thursday, March 31, 2016

[​IMG]

Tanzania tutegemee kuingia kwenye shida ya kiuchumi. Wale washirika wetu wa maendeleo yaan zile nchi za ulaya. Kwa kauli ya pamoja wamesitisha misaada katika nchi yetu.

Tukumbuke misaada yao inaingia moja kwa moja kwenye bajet!! Wanaojua hatujitoshelezi. Kimaneno tunajitosheleza kwa 60% kivitendo hatuzid 40%.Ni zaid ya ile MCC. Maamuzi hayo yamekubaliwa na nchi 10 kati ya 14 za Umoja wa ulaya.

Swali kwa watawala hata hizo milijua hamtapewa mlijiandaa kujitegemea?

Maana ya MCC nilimsikia msemaji wa wizara ya fedha anasema waljua haztakuja hawakuziweka kwenye bajeti.

Je na za washirika wa maendeleo hamkuziweka???

Wananchi mnatwambia tufunge mikanda suruali zetu zinavyotupwaya wakati nyie mnashindwa Hata kufunga vifungo vya makoti kwa vitambi.

[​IMG]

Kundi la watoa misaada 10 kutoka nchi za magharibi wametangaza kusitisha ufadhili wao kwa bajeti ya serikali ya Tanzania.

Hii inafuatia uamuzi wa shirika la utoaji misaada la serikali ya marekani kuondoa msaada wa dola 472 wa kufadhili miradi ya maendeleo kutokana na jinsi uchaguzi wa kisiwa cha Zanzibar ulivyoendeshwa.

Karibu theluthi moja ya bajeti ya Tanzania ilitegemea msaada mwaka uliopita, kwa hivyo hatua hizo za hivi punde ni pigo kwa mipango ya maendeleo ya serikali mpya.

BREAKING NEWS: MH: LOWASSA YAMKUTA MZITO, "CHID BENZ" AAMUA KUTUMBUA MAKUBWA TENA BILA WOGA

20160322_043137

HAYA NDIO YALIYOJILI MUDA SI MREFU: CHAMA CHA WANANCHI (CUF) CHATOA TAMKO ANGALIZO NA KUTAMKA HAYA

Maalim Seif Sharrif Hamad, aliyekuwa mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CUF, nyuma ni wafuasi wake

CHAMA cha Wananchi (CUF) kinahofia mauaji visiwani Zanzibar endapo kitatoa kauli ya kuwataka wanachama na wananchi kusaka haki yao kutoka mikononi mwa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), anaandika Happyness Lidwino.    
Nassor Ahmed Mazrui, Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar akizungumza na mtandao huu leo amesema, CUF ina hofu ya Mungu na kwamba, wanajua endapo watakapowafungua minyororo wananchi wao, Zanzibar haitakalika.
Amesema, chama hakioni hoja ya kusababisha mauaji kutokana na dhuluma inayofanywa na Dk. Ali Mohammed Shein, Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar na viongozi wa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
“Dunia ukiiendea mbio mwisho wake ni kuangamia, tunajua dhulma huwa haidumu. Inahitajika sana subra ili kuokoa maisha ya wengi. Tunajua kwamba dhulma imetendeka lakini hakuna shaka hakutakuwa na mwananchi atakayeuawa kwa sababu yetu,” amesema na kuongeza;
‘’Sisi tumetulia, hatuna shaka tunatizama tu watakachoamua kufanya sisi tutakaa kimya kwani hatuko tayari wananchi wetu wamwage damu.”
Mazrui amesema kuwa, kwa sasa wananchi wengi wanaweza kutojua kwanini CUF imekaa kimya na kwamba “kukaa kimya pia si ujinga, muda ukifika wananchi wataelewa kwa nini tuliamua kujitoa kwenye uchaguzi na kukaa kimya.’’
Magdalena Sakaya, Naibu Katibu Mkuu wa CUF Bara ameuambia mtandao huu kuwa, wananchi watulie kwakuwa chama chao hakitayumba.
Amesisitiza kwamba, CCM sio mbabe isipokuwa busara na muono wa mbali wa CUF ndio mafanikio ya uchaguzi unaofanyika leo na kwamba, chama chao hakirudi nyuma katika harakati zake mwaka 2020.
“Hakuna marefu yasiyo na nchi,” amesema Sakaya na kuongeza “ wakati wa CCM kuachia nchi unafika, hili halipingiki. Tunajua wananchi hawatuelewi lakini watatuelewa.”
Kuhusu uendeshwaji wa chama Sakaya amesema, “kwa asilimia kubwa chama kinaendeshwa na wananchi wenyewe na ruzuku inayopatikana ni ndogo sana kwa hiyo chama kitaendelea kuwa imara hata kama ruzuku itapungua.”
Kuhusu hatua zitakazochukuliwa na chama baada ya kumalizika kwa uchaguzi Sakaya amesema, hivi sasa chama kipo kimya kikisubiriwa ‘rais wao haramu’ atangazwe kisha kitajua ni hatua gani za kuchukuliwa kwa kuwa hadi sasa pia kuna baadhi ya viongozi wao wapo kizuizini.
‘’Serikali na CCM hadi sasa bado hawaamini kama wanaendesha uchaguzi wao wa mabavu salama kwa kuwa, wanachokifanya sio kizuri hakiwapendezi wananchi ndio maana walikuwa wanajihami kwa kuleta vifaa vya vita hata kuwakamata viongozi wetu wakihofia wanaweza kuvuruga uchaguzi,” amesema Sakaya.

BREAKING NEWSSSSSSSSS KUTOKA CLOUDS STATION


RONALDO AONGOZA USHINDI WA URENO VS BELGIUM

Wednesday, March 30, 2016

Cristiano 7

Cristiano Ronaldo kwa mara nyingine alikuwa kwenye kiwango cha juu baada ya kuisaidia timu yake ya taifa kupata ushindi wa magoli 2-01 kwenye mchezo wa kirafiki dhidi ya Ubelgiji uliopigwa Jumanne usiku.
Ndani ya dakika 10 za kwanza, Ronaldo alifanya shambulio la hatari lililomuacha hoi beki wa Ubelgiji Jason Denayer.
Ronaldo alitengeneza nafasi mbili za kupachika bao laikini timu yake ilishindwa kufanya hivyo kutokana na uimara wa golikipa wa Chelsea na timu ya taifa ya Ubelgiji Thibaut Courtois.
Hatimaye Ureno ilipata bao dakika ya 20 lililofungwa na Nani kabla ya Cristiano Ronaldo kupachika bao la pili dakika tano kabla ya kwenda mapumziko.
The Real Madrid superstar headed home from a João Mário cross and celebrated in typical style.
Cristiano 71
Superstar huyo wa Real Madrid alifunga bao lake kwa kichwa akiunganisha krosi ya João Mário kisha kushangilia kwa style ya aina yake. Hilo ni bao la 47 kwa Cristiano Ronaldo msimu huu.
Romelu Lukaku aliifungia Ubelgiji goli la kufutia machozi akiunganisha kwa kichwa krosi ya mdogoake Jordan Lukaku.
Lukaku Jordan

NIGERIA NJE AFCON 2017, NAFASI YA TANZANIA IKOJE?

Egypt vs Nigeria

Nigeria wameshindwa kufuzu kwa fainali za mataifa ya Afrika (Africa Cup of Nations) mwaka 2017 nchini Gabon baada ya kuchezea kichapo cha bao 1-0 mbele ya Misri kwenye mchezo wa kundi G mechi iliyopigwa Jumanne usiku.
Wakiwa wamebakiza mchezo mmoja mkononi, huku kinara wa kundi ndiye anayefuzu kwenye michuano hiyo, Nigeria haina nafasi tena ya kwenda Gabon. Endapo Nigeria itashinda mchezo wake wa mwisho dhidi ya Tanzania itafikisha pointi 5 wakati tayari Misri inapointi saba mkononi ikiongoza kundi G.
Goli la Ramadan Sobhy la dakika ya 65 limeiweka Misri kwenye nafasi nzuri ya kufuzu kucheza fainali za mataifa ya Afrika mwaka 2017.
Tanzania itaialika Misri mwezi June na Misri watajihakikishia kukata tiketi ya Gabon kwa matokeo yoyote isipokuwa kama watapoteza mchezo huo kwa magoli 3-0.
Nigeria ilitwaa ubingwa wa Cup of Nations mwaka 2013 lakini sasa wameshindwa kufuzu kwenye michuano hiyo kwa mara ya pili mfululizo
Nigeria ilijitahidi kutafuta goli la kusawazisha na ilikaribia kufanya hivyo pale winga wa West Ham Victor Moses alipoachia shuti kali dakika ya 84 likagonga mwamba.
Mchezo huo uliopigwa Alexandira ulikuwa wa kufa na kupona kwa Nigeria baada ya Chad kujitoa kwenye kundi G kuwania kufuzu kushiriki fainali hizo kwa sababu ya hali ngumu ya kiuchumi na kusababisha matokeo yote ya awali yaliyoihusisha timu hiyo kufutwa.
Hatua hiyo ya Chad kujitoa imepelekea kubaki timu tatu kwenye kundi G na kwa mujibu wa kanuni za CAF timu itakayoongoza kundi ndiyo itafuzu moja kwa moja kushiriki fainali zijazo.
Misri ina pointi saba huku ikiwa na mechi moja mkononi dhidi ya Tanzania iliyo nafasi ya mwisho kwenye kundi ikiwa na pointi moja lakini inamichezo miwili ya kucheza.
Ili Tanzania iweze kufuzu kucheza fainali zitakazofanyika Gabon mwaka 2017, inahitaji ushindi usiopungua magoli 3-0 dhidi ya Misri sawa na yale ambayo ilifungwa na Misri mwezi June mwaka uliopita timu hizo zilipokutana kwasababu matokeo ya head-to-head yatatumika kuamua ni timu ipi itafuzu endapo timu zitamaliza zikiwa na pointi sawa kwenye kundi husika.
Wakati huohuo Tanzania itahitaji ushindi mwingine kwenye mchezo wao wa mwisho dhidi ya Nigeria mwezi September mwaka huu.

SERIKALI YAKINUKISHA USIKU HUU YAFUTA USAJILI MASHIRIKA 110 NA HII NDIO ORODHA YA MASHIRIKA YALIYOFUTWA


Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali amefuta usajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiesrikali (NGOs) 109 kwa kuendesha shughuli zao kinyume cha Sheria ya NGOs Na. 24 ya mwaka 2002 kama ilivyorekebishwa mwaka 2005. Mashirika hayo ni yale ambayo hayajawasilisha taarifa za mwaka kwa kipindi cha miaka miwili pasipo kutoa sababu za msingi, kutolipa ada ya mwaka au kuendesha shughuli za NGOs bila kusajiliwa chini ya Sheria ya NGOs.
Kwa taarifa hii, Mashirika yaliyotajawa hapa chini yamefutiwa usajili na yataarifiwa kusitisha shughuli zao kuanzia tarehe ya tangazo hili (30/03/2016). Baada ya kipindi hicho, Msajili wa NGOs atayachukulia hatua stahiki Mashirika ambayo yatakaidi amri hii na kuendelea na shughuli za NGOs kinyume na Sheria husika.
MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI (109) YALIYOFUTIWA USAJILI KUANZIA TAREHE 30/3/2016  NI KAMA IFUATAVYO:

1.             THE MEDICAL WOMEN ASSOCIATION OF TANZANIA (MEWATA)
2.             AFRICAN GENDER AND GOOD GOVERNANCE ALLIANCE
3.             AFRICAN WILDLIFE FOUNDATION
4.             AGENDA FOR ENVIRONMENTAL AND SUSTAINABLE DEVELOPMENT
5.             ANTIOKIA MISSION INTERGRATED SOCIAL DEVELOPMENT
6.             BUSEGWE DEVELOPMENT ASSOCIATION
7.             BUTIAMA DEVELOPMENT ASSOCIATION
8.             CARE FOR THE CHILD (CFC)
9.             CHAKUFAA DEVELOPMENT FOUNDATION
10.          CHAMA CHA KUSAIDIA WATOTO YATIMA MAKAMBAKO
11.          COMFORT WOMEN RELIEF FOUNDATION
12.          COMMUNITY AGRICULTURAL ACTION SERVICES CENTRE
13.          COMMUNITY SERVICES SUPPORT OF TANZANIA (COSESU-T)
14.          DAUGHTERS OF ZION FOUNDATION LTD
15.          DEFENCE OF HUMAN RIGHTS CITIZEN RIGHTS
16.          DEVELOPERS OF SUSTAINABLE COMMUNITY BASED ACTIVITIES (DESCOBA)
17.          DIANA WOMEN EMPOWERMENT ORGANIZATION
18.          EDNA DEVELOPMENT FOUNDATION
19.          EMPOWERMENT AGAINST POVERTY AND HIV/AIDS
20.          EMPOWERMENT FOR THE DISADVANTAGED COMMUNITY (EDC)
21.          ENVIRONMENTAL MANAGEMENT AND NUTRITIONAL SERVICES AGENCY (EMA-NUSA)
22.          GLOBAL VISION TANZANIA (GVT)
23.          GRASSROOTS INITIATIVE FOR YOUTH AND ELDERLY DEVELOPMENT ORGANIZATION (GIYEDO)
24.          HOPE MISSION OF DEVELOPMENT FOR THE DISABLED (HOMIDED)
25.          HURUMA CHILD MINISTRY CENTRE
26.          HURUMA REHABILITATION PROGRAMME
27.          IMANI WOMEN ECONOMIC EMPOWERMENT ASSOCIATION (IWEA)
28.          INTERNATIONAL MEDICAL CORPS
29.          IZAAZ MEDICAL PROJECT
30.          JUMUIYA EDUCATION BAGAMOYO (JEBA)
31.          JUNIOR ACHIEVEMENT OF TANZANIA
32.          KAMACHUMU IN NGEMU AGENDA (KINGA)
33.          KILIMO HAI TANZANIA (KIHATA)
34.          KUZA EDUCATION DEVELOPMENT
35.          MANDATE AFRICA FOUNDATION
36.          MASASI FARMERS ADVOCACY ASSOCIATION (MAFADA)
37.          MAZINGIRA INSTITUTE OF TANZANIA (MAI-TANZANIA)
38.          SUMBAWANGA ESCARPMENT ENVIRONMENTAL CONSERVATION ORGANIZATION (SEECO)
39.          MFUKO WA MAENDELEO YA WAISLAM MKOA WA RUVUMA
40.          MKONGO MLOKA DEVELOPMENT ASSOCIATION
41.          MOROGORO ENVIRONMENTAL CONSERVATION ACTION GROUP
42.          MOROGORO ENVIRONMENTAL CONSERVATION ACTION GROUP
43.          MUUNGANO DEVELOPMENT ASSOCIATION (MUDEA)
44.          MWAKALELI COMMUNITYDEVELOPMENT ORGANIZATION (MWACODO)
45.          MWALIMU NYERERE UWC FOR SELF RELIANCE
46.    MWANANYAMALA WOMEN LDEVELOPMENT GROUP (MWAWODE)
47.          NATIONAL LIFE DEVELOPMENT ASSOCIATION
48.          NJOMBE DEVELOPMENT ORGANIZATION (NDO)
49.          NORWEGIAN PEOPLE AID
50.          OLOF PALME ORPHANS CENTRE
51.          DEVELOPMENT AGENCY PROBATION TIME RESEARCH
52.          PANGOLIN ELITE SPORTS FOUNDATION
53.          PARTGAGE TANZANIA
54.          PERIPHERY AREAS DEVELOPMENT ASSOCIATION (PADA)
55.          POVERTY ALLEVIATION AND AGRICULTURAL DEVELOPMENT (PADEFO)
56.          POVERTY FIGHTERS AND CHARITABLE GROUP
57.          POVERTY FIGHTERS AND DEVELOPMENT SOCIETY OF TANZANIA (POFIDESO)
58.          PRICESS AGNES FOUNDATION
59.          PROGRESS ASSOCIATION TANZANIA (PATA)
60.          PROMOTION OF FARMING AND ORPHANS EDUCATION IN TANZANIA (PROFOET)
61.          RESTE YOUTH TRAINING TRUST FUND
62.          RIDHIKA SHIRIKA LA ULINZI NA MAZINGIRA
63.          RURAL ACCESS TECHNOLOGY INORMATION AND INSTITUTIONAL SERVICES (RATHS)
64.          RURAL FAMILY LIFE PLANNING ASSOCIATION
65.          RURAL INITIATIVES FOR DEVELOPMENT OF TANZANIA – RIDE(T)
66.          RURAL ORIENTED SUSTAINABLE DEVELOPMENT ORGANIZATION (ROSDO)
67.          RURAL WOMEN DEVELOPMENT ASSOCIATION
68.          SAMORSES EDUCATION FOUNDATION
69.          SANTA MERINA EDUCATION FOUNDATION
70.          SAVE LIFE ASSOCIATION
71.          SHINYANGA FOUNDATION FUND (SFF)
72.          SOCIETY FOR RURAL DEVELOPMENT INITIATIVES (SRDF)
73.          SOLIDARITY WOMEN GROUP (SWG)
74.          SOLUTION AND OPPORTUNITIES FOR DISADVANTAGED IN AFRICA (SODA)
75.          SOUTH DEVELOPMENT IN TANZANIA (YODIT)
76.          SUSTAINABLE INTERGRATED FARMING AND HEALTH IMPROVEMENT
77.          TAMADA
78.          TANZANIA ACTION FOR PASTORAL EDUCATION ADVOCACY (TACEA)
79.          TANZANIA ASSOCIATION OF ENVIRONMENTAL ENGINEERS (TAEES)
80.          TANZANIA DEVELOPMENT AND AIDS PREVENTION (TADEPA)
81.          TANZANIA GIRL’S EMPOWERMENT (TAGE)
82.          TANZANIA HURUMA AIDS ORGANIZATION (THAO)
83.          TANZANIA INITIATIVES FOR POVERTY ALLEVIATION (TIPA)
84.          TANZANIA JOURNALIST ASSOCIATION (TAJA)
85.          TANZANIA MANGROVE PROTECTION ASSOCIATION (TAMPA)
86.          TANZANIA MARGINALIZED AREAS COMMUNITY SERVICES FOUNDATION
87.          TANZANIA ROAD ASSOCIATION (TRA)
88.          TANZANIA SOCIETY FOR THE BLIND (TASODEB)
89.          TANZANIA SUPPORT AND TRAINING YOUTH AND WIDOWS ASSOCIATION
90.          TANZANIA TENANTS ASSOCIATION
91.          TANZANIA YOUTH MUSLIM ASSOCIATION (TAYMA)
92.          TARIME – SIRARI GROUP (TARSI)
93.          TAX SERVICES TANZANIA
94.          TECHNOWLEDGE TANZANIA (TKTZ)
95.          TELECOMS AND ELECTRONICS TECHNICIANS ASSOCIATION (TETA)
96.          TEMEKE DISTRICT YOUTH FOUNDATION (TEYOFO)
97.          THE HUMAN DEVELOPMENT PROJECTS AND TANZANIA
98.          NAMTUMBO NETWORK OF CIVIL SOCIETY (NANECISO)
99.          THE SURVIVAL AFRICA TRUST (SAT)
100.      THE TANZANIA HERALDS YOUTH SERVICES (THEYS)
101.      THE VOICE OF THE AIDS AND ORPHANS (VOTAO)
102.      THE WOMEN WIDOW CHILDREN AND FISHERIES DEVELOPMENT
103.      TUMAINI ORPHANS AND VULNERABLE CHILDREN CENTRE
104.      UMOJA WA DOUYA NA MAKANGAWE (UDOMA)
105.      UMOJA WA MADEREVA WA MABASI TANZANIA (UWAMATA)
106.      WATOTO CARE ORGANIZATION (WACO)
107.      WOMEN AND YOUTH ECONOMIC DEVELOPMENT INITIATIVE (WOYEDE)
108.      WOMEN DEVELOPNMENT AND GENDER
109.      SAIDIA JAMII YA WAZEE KAGERA SAJAWAKA)

110.      UKIMWI ORPHANS ASSISTANCE (UKOA)
Imetolewa na,
M.S. Katemba
MSAJILI WA NGOs
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO
29 Machi, 2016
 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU