ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

Ugiriki:Wasusia mechi kupinga vifo vya wahamiaji

Sunday, January 31, 2016


Wachezaji wa timu mbili hasimu nchini Ugiriki wamesusia mechi wakipinga ongezeko la vifo vya wahamiaji wanaozama wakijaribu kuingia nchioni humo kukwepa vita Syria na Iraq.
Wachezaji hao wa timu ya AEL Larissa na wenzao wa timu ya Acharnaikos waliketi chini pindi refarii alipopuliza kipenga cha kuanzwa kwa mechi hiyo ya ligi.
Tukio hilo lililodumu kwa zaidi ya dakika mbili lilimwacha muamuzi asijue la kufanya!
Hata ta hivyo alipoulizia cha mno akaelezewa kuwa muda mchache kabla ya mechi hiyo taarifa zilichipuka kuwa zaidi ya wahamiaji wengine 39 walikuwa wamekufa maji wakijaribu kuingia nchini humo wakitoroka vita.
Taarifa hiyo iliwaudhi sana na kuwachochea kuchukua hatua hiyo.
Wahamiaji hao walikuwa wametokea Uturuki wakijaribu kufika katika moja ya visiwa vya Ugiriki lakini mawimbi makali yakaifanya mtumbwi walimokuwa kuzama majini.
Timu ya AEL Larissa ilisema kuwa wachezaji wao walichukua hatua hiyo wakijaribu kuangazia macho ya ulimwengu na kila awaye yote kwa tatizo hilo la wahamiaji ambao wanazidi kufa maji kila kukicha wakitoroka vita.
Idadi kubwa ya wale wanaopoteza maisha yao baharini ni watoto wanawake na wazee.

Samatta atambulishwa rasmi Genk Ubelgiji

Samatta
Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Tanzania Mbwana Samatta ametambulishwa kama mchezaji mpya wa klabu ya Genk ya Ubelgiji.
Samatta amejiunga na klabu hiyo inayocheza Ligi Kuu ya Ubelgiji kutoka kwa TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Samatta, aliyetawazwa mchezaji bora wa mwaka Afrika 2015 kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani, ametia saini mkataba wa hadi mwisho wa msimu wa 2019/2020.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 23, ambaye pia hucheza kama winga, alishinda vikombe sita vikubwa akiwa na TP Mazembe, ikiwa ni pamoja na kushinda Ligi ya Klabu Bingwa Afrika mwaka 2015.
Ameichezea timu ya taifa mara 20 na kufunga magoli saba.
Samatta
Akiandika kwenye akaunti yake ya Twitter, Samatta alisema: “Nimejiunga rasmi na<span >@KRCGenkofficial. Nasubiri kwa hamu kipindi hiki kipya maishani mwangu.”
Alimshukuru mmiliki wa TP Mazembe Bw Moise Katumbi na mashabiki kwa kumuunga mkono.

MAJALIWA AHUDHURIA IBADA YA KUMUINGIZA KAZINI MKUU WA KKKT TANZANIA ASKOFU SHOO MJINI MOSHI

4
Waziri MkuuKassim Majaliwa  akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa katika ibada ya kumuingiza kazini Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Askofu Frederick Shoo kwenye kanisa Kuu la KKKT mjini Moshi Januari 31, 2016.
1
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea picha aliyopewa na Askofu Mkuu Mpya wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheli,Askofu  Frederck Shoo katika ibada ya kumuingiza kazini askofu huyo ilyofanyika kwenye kanisa kuu la KKKT mjini Moshi Januari 31, 2016.
3
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizunguza katika ibada ya kumuingiza kazini Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Frederick Shoo iliyofanyika kwenye kanisa Kuu la KKKT mjini Moshi Januari 31, 2016.
5
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akizungumza na Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Frederick Shoo (kulia) na Askofu Mkuu wa KKKT Mstaafu Alex Malasusa baada ya ibada ya kumuingiza kazini Askofu Shoo iliyofanyika kwenye Kanisa Kuu la KKKT mjini Moshi Januari 31, 2016.

(PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU)

Chelsea na West Brom watozwa faini

Wednesday, January 27, 2016


Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya Uingereza, Chelsea na West Brom wametozwa faini kwa utovu wa nidhamu uwanjani katika mechi iliyozongwa na ubishi mwezi uliopita.
Shirikisho la soka nchini Uingereza FA limeitoza Chelsea faini ya pauni £65,000.
West Brom kwa upande wake imepigwa faiani ya pauni £35,000.
Mshambulizi mbishi wa Chelsea Diego Costa alihusika katika mengi ya makabiliano hayo uwanjani.
Mhispania huyo alishambuliana na kiungo cha kati wa West Brom, Claudio Yacob baada ya kuangushwa.
West Brom walijifurukuta kutoka nyuma na kutoka sare na wenyeji wao Stamford Bridge.
Katika taarifa kwa vyombo vya habari FA inasema kuwa timu zote mbili zilishindwa kudhibiti wachezaji wake.
Yacob, ambaye alikuwa keshaoneshwa kadi ya njano kwa kumuangusha Costa, aliondolewa uwanjani na kocha Tony Pulis.
Siku chache baadaye kocha wa muda wa Chelsea Guus Hiddink alielezea kutoridhika na uamuzi wa refarii Anthony Taylor, akisema kuwa alipaswa kumuonesha kadi nyekundu Yacob.

Azam,Simba,Yanga zasonga 16 bora


Timu za Azam FC, Simba SC, Yanga zimeungana na timu nyingine saba kufuzu kwa hatua ya 16 Bora ya michuano ya Kombe la Shirikisho .
Michezo ya mzunguko wa nne ikitarajiwa kuchezwa mwishoni mwa mwezi Februari,
Jumla ya michezo 10 mpaka sasa imeshachezwa na timu kumi kujikatia tiketi ya kucheza mzunguko wa nne, ambao utazikutanisha jumla ya timu 16 mwezi ujao kusaka timu nane zitakazosonga mbele hatua ya nane bora.
Timu zilizofuzu hatua ya 16 bora mpaka sasa ni Azam FC, JKT Mlale, Mwadui FC, Ndanda FC, Panone FC, Rhino Rangers, Simba SC, Tanzania Prisons, Toto Africans na Young Africans.
Bingwa wa michuano ya Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) mwaka huu, ataiwakilisha Tanzania mwaka 2017 kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika CAF

Kampuni ya Magazeti ya Mwananchi Yakanusha Kujihusisha na Biashara ya Kusafirisha Wahamiaji Haramu

Idadi ya Raia wa kigeni kutoka nchini Ephiopia waliokuwa wakisafirishwa na Gari la magazeti la kampuni ya Mwananchi Communication Ltd imefikia 12 baada ya wengine 4 kukamatwa Jioni wakiwa Eneo la Kibwabwa  mjini Iringa wakiwa wamefichwa porini.
 
Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Iringa Peter Kakamba amesema kuwa tayari ametuma usafiri kwenda kuwabeba Raia hao ambao wanadai walishushwa katika gari hilo aina ya Hiace ili kuvuka eneo la ukaguzi wa Magari ( check pointi)  kijiji cha Igumbilo nje kidogo ya mji wa Iringa.

Wakati huo huo Kampuni ya Mwananchi Communication Limited (MCL)  imetoa ufafanuzi kuhusiana na kuhusishwa na kadhia hiyo. Soma zaidi:

Usajili Ulaya Ulimwengu akamilisha mazungumzo na St.Etienne.

Saturday, January 23, 2016

http://globalpublishers.co.tz/wp-content/uploads/2015/11/url.jpg
Wakati Mbwana Samata akiwekewa vikwazo kuondoka TP Mazembe, hali ni tofauti kwa Thomas Ulimwengu, ambaye yeye mambo yamemnyookea.
Mshambuliaji wa Klabu ya TP Mazembe, Thomas Ulimwengu ameshakamilisha mazungumzo na Klabu ya Saint Etienne ya Ufaransa na kinachosubiriwa ni yeye kusaini mkataba wa kujiunga na klabu hiyo.
Ulimwengu amesema kabla ya dirisha dogo la usajili barani Ulaya kufungwa mwezi ujao tayari atakuwa ameshatua Ufaransa kuanza maisha mapya ya kusakata kandanda barani ulaya.
Ulimwengu ameileza StarTv kuwa mmiliki wa TP Mazembe, Mose Katumbi amebariki kuondoka kwake.
Ulimwengu ameweka bayana kuwa amechagua kwenda Saint Etienne kwa kuwa klabu hiyo inamsajili moja kwa moja bila kufanya majaribio.
Klabu ya Saint Etienne inayoshiriki ligi kuu nchini ufaransa kwa sasa inashika nafasi ya 5 katika msimamo wa ligi hiyo, ikiwa nyuma ya point 4 na timu ya Monaco inayoshika nafasi ya pili na point 34.
Hii ni kusema kwamba kama dili la Ulimwengu litakamilika na Saint Etienne ikamaliza nafasi ya tatu za juu basi Thomas Ulimwengu atakua Mtanzania wa kwanza kushiriki michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya yaani UEFA CHAMPIONS LEAGUE.

Rais Magufuli amteua Kikwete kuwa mkuu wa chuo kikuu cha dar es salaam

WEZI WA MALI YA UMMA ! RAIS MAGUFULI KUTUMBUA MAJIPU YOTE MPAKA YAISHE

Friday, January 22, 2016

Rais John Magufuli akicheza ngoma ya kimasai pamoja na wananchi muda mfupi baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) jana, akiwa njiani kwenda Arusha kwa ziara ya kikazi. 

RAIS John Magufuli ametoa mwito kwa Watanzania kumuombea ili aendelee kuwashughulikia wote wanaofanya ubadhirifu wa fedha za umma kupitia kampeni yake ya kutumbua majipu. 

“Nataka niwahakikishieni kuwa nitaendelea kutumbua majipu yote mpaka yaishe, na naomba mniombee ili kazi hii ya kutumbua majipu ifanyike kwa mafanikio,” alisema Dk Magufuli. 

Alitoa kauli hiyo wakati alipokuwa akizungumza na wananchi katika mikoa ya Kilimanjaro na Arusha jana, alipotua kwa ziara ya kikazi ikiwa ni ya kwanza kwao tangu achaguliwe kushika wadhifa huo Novemba 5, mwaka jana. 

Dk Magufuli aliwasili mkoani Arusha, ambako kesho atatunuku Kamisheni kwa maofisa wanafunzi wa kundi la 57/15 katika Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi (TMA) Monduli mkoani hapa. 

Rais Magufuli aliwasili mjini Arusha akitokea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), alikotua kwa ndege akitokea jijini Dar es Salaam na kupokewa na mamia ya wananchi. Akiwa uwanjani hapo, Rais Magufuli aliwashukuru wananchi kwa mapokezi makubwa aliyoyapata na aliwaeleza kuwa uchaguzi umekwisha, kilichobaki ni kazi tu. 

“Nawashukuru sana ndugu wananchi kwa mapokezi haya makubwa, naomba kuwahakikishia kuwa uchaguzi umekwisha na sasa kilichobaki ni kuchapa kazi tu,” alisema Rais Magufuli. 

Akiwa njiani kutoka KIA, Rais Magufuli alisimamishwa na wananchi wa njiapanda ya KIA, Kikatiti, Usa River, Tengeru na Mount Meru mjini Arusha ambako huko kote pamoja na kusisitiza kuwa uchaguzi umekwisha na kilichobaki ni kuchapa kazi, aliwahakikishia kuwa hatawaangusha. 

Aidha, Rais Magufuli alisema tayari serikali imeanza kutoa fedha kwa ajili ya kugharimia elimu ya msingi na sekondari baada ya kufuta ada na alionya kuwa watumishi wa umma hususani wakuu wa shule watakaothubutu kufanya ubadhirifu wa fedha hizo watashughulikiwa. 

Alisema yote aliyoyaahidi kwa wananchi wa mkoa wa Arusha na Watanzania kwa ujumla, ikiwemo ujenzi wa barabara za Arusha, kulipa fidia za wananchi na kufuta ada ya shule za msingi na sekondari yanatekelezwa. 

Rais Magufuli alisisitiza kuwa serikali yake haitawabagua Watanzania kwa dini zao wala makabila yao na wala haitawabagua kwa misingi ya vyama vyao na kanda zao. Aliwataka Watanzania wote kuiweka mbele Tanzania na kushirikiana kuiendeleza.

Ligi Kuu TZ imesimama, ila hii ndio burudani ya soka weekend hii mtu wangu, sio ya kukosa …


Mtu wangu wa nguvu mzunguuko wa kwanza wa Ligi Kuu soka Tanzania bara umemalizika, lakini haina maana kwamba weekend hii hakuna burudani ya soka, kuna michezo kadhaa ya Kombe la FA kwa Tanzania, Ligi Kuu Uingereza na Hispania. Hii ndio ratiba ya michezo yenyewe mtu wangu.
Kesho Jumamosi ya January 23 michezo mitatu itachezwa, mjini Morogoro Burkinfaso FC watawakaribisha Simba SC katika uwanja wa Jamhuri mjini humo,  Pamba FC watawakaribisha Toto Africans uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, huku Ndanda FC wakicheza dhidi ya Mshikamno FC katika uwanja wa Nagwanda Sijaona Mtwara.
Jumapili ya January 24 michuano hiyo itaendelea kwa michezo mitatu, jijini Dar es salaam Young Africans watawakaribisha Friends Rangers uwanja wa Taifa, Njombe Mji watakuwa wenyeji wa Tanzania Prisons uwanja wa Amani Njombe, huku Stand United wakicheza dhidi ya Mwadui FC katika uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.
Hii ni ratiba ya Ligi Kuu Uingereza weekend hii
2
Jumamosi ya January 23 kwa saa za Afrika Mashariki
  • Norwich Vs Liverpool Saa 15:45
  • Crystal Palace Vs Tottenham Saa 18:00
  • Leicester Vs Stoke Saa 18:00
  • Man Utd Vs Southampton Saa 18:00
  • Sunderland Vs Bournemouth Saa 18:00
  • Watford Vs Newcastle Saa 18:00
  • West Brom Vs Aston Villa Saa 18:00
  • West Ham Vs Man City Saa 20:30
Jumapili ya January 24 ratiba kwa saa za Afrika Mashariki
  • Everton Vs Swansea Saa 16:30
  • Arsenal Vs Chelsea  Saa 19:00
Ratiba ya Ligi Kuu Hispania
wer
Ratiba ya Ligi Kuu Hispania kwa saa za Afrika Mashariki Jumamosi ya January 23
  • Málaga Vs Barcelona Saa 18:00
  • Espanyol Vs Villarrea Saa 20:15
  • Granada CF Vs Getafe Saa 22:30
  • Rayo Vallecano Vs Celta de Vigo Saa 00:05
Jumapili ya January 24
  • Ath Bilbao Vs Eibar Saa 14:00
  • Atl Madrid Vs Sevilla Saa 18:00
  • Deportivo de La Coruña Vs Valencia Saa 20:15
  • Real Betis Vs Real Madrid Saa 22:30

KAMATI YA KURATIBU MISS TANZANIA YAJITOA KWENYE MASHINDANO


PI1

Mwenyekiti wa Kamati ya kuratibu Miss Tanzania Juma Pinto akiongea na waandishi wa habari(hawapo pichani) leo  jijini Dar-es-Salaam juu ya kujitoa kwao kama kamati ya kuratibu Miss Tanzania ambayo ilichagulia na kampuni ya Lino International Agency, kushoto ni Msemaji wa kamati hiyo Joketi Mwegelo na kulia ni Mjumbe wa kamati Gladys Shao 

PI3

Waandishi wa habari wakimfuatilia kwa makini Mwenyekiti wa Kamati ya kuratibu mashindano ya Miss Tanzania, Juma Pinto (hayupo pichani) alipokuwa akitoa sababu za kujitoa kwa kamati katika mashindano hayo.
PICHA NA Beatrice Lyimo-Maelezo
………………………………………………………………………………………………………………….
Lilian Lundo- Maelezo
Dar es Salaam.

Kamati ya kuratibu Miss Tanzania imejitoa rasmi kusimamia mashindano ya Miss Tanzania kuanzia leo tarehe 21/01/2016.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo  Juma Pinto alisema hayo leo, alipokuwa akiongea na waandishi wa habari jijini Dar-es-Salaam.
“Tumekuja
kutoa taarifa kwamba, kama tulivyo teuliwa na kampuni ya Lino International Agency, kuandaa, kuendesha na kusimamia mashindano ya Miss Tanzania, kamati yangu imeamua kujitoa kutokana na majukumu ya kamati kuingiliwa na kampuni ya Lino,” alisema Pinto.
Pinto aliongeza kwa kusema kuwa kamati yake ilipewa jukumu la kuendesha mashindano na kuwajibika kufanya kila kitu na Lino itakuwa kama washauri, lakini badala yake Lino imetaka kuhodhi majukumu yote na kamati ikawa ni ya kutafuta wadhamini.

Kamati hiyo imefanya vikao vingi vya kuhakikisha mashindano yanaboreshwa na kubadilisha mfumo ili kuifanya Miss Tanzania kuwa na mwonekano tofauti kama ambavyo Lino ilivyoamua kuweka kamati mpya ili kuboresha mashindano hayo.
Kutokana na kutopata muafaka katika vikao hivyo vya kuboresha mashindano ya Miss Tanzania, Kamati ya kuratibu mashindano hayo kwa nia njema na wala si kwa ubaya imeamua kujitoa katika Mashindano hayo.

Aidha, Pinto amewaomba radhi wadhamini ambao wameshaongea nao kama kamati na walioonesha nia ya kuwasaidia, amewataka kuendelea kufanya mawasiliano na kampuni ya Lino kwani madhumuni ni kudhamini mashindano na sio kamati.

CHAN: Tunisia yatoka sare na Nigeria

Tunisia

Mechi za mkumbo wa pili Kundi C katika michuano ya kombe la taifa bingwa Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani zimemalizika kwa klabu zote kutoshana nguvu.
Nigeria walitangulia kwa kutoka sare ya 1-1 na Tunisia mjini Kigali.
Bao la Nigeria lilitingwa wavuni na Elvis Chikatara dakika ya 51.
Tunisia walihakikisha wanaondoka na alama moja baada ya kusawazisha kupitia Ahmed Akaichi dakika ya 69. Akaichi alikuwa ametumbukiza mpira kimiani kwa kichwa dakika ya kwanza lakini alikuwa ameotea.
Kwenye mechi ya pili, Issa Moussa alifungia Niger bao la kwanza nao Guinea wakapata lao kupitia Alseny Camara.
Ammadou Issa, aliyekuwa ameingia uwanjani kama nguvu mpya, aliweka Niger kifua mbele dakika ya 49.
Aboubacar Bangoura hata hivyo alikomboa bao hilo na mambo yakasalia hivyo hadi kipenga cha mwisho kilipopulizwa.
Kwa sasa Nigeria wanaongoza kundi hilo na alama nne, Tunisia na Guinea wakifuata wakiwa na alama mbili kila mmoja, nao Niger inavuta mkia ikiwa na alama moja pekee.
Mechi za mwisho Kundi C zitachezwa Jumanne wiki ijayo ambapo Nigeria watacheza dhidi ya Guinea nao Tunisia wacheze dhidi ya Niger.

ETC VISUAL PRODUCTION NA PUNGUZO KUBWA KWA WASANII WA NJOMBE

Saturday, January 16, 2016

ETC VISUAL PRODUCTION wakiwa kama wataalamu wa kutengeneza kazi zenye ubora wa hali ya juu sana (HIGH DIFINITIONS) wanapenda kuwa tangazia watanzania wote kuwa kwa mwaka wanapunguza kubwa sana kwa wale wanao hitaji kufanya kazi na kampuni yetu.

Kazi zinazofanywa na kampuni ni pamoja na kuandaa nyimbo za picha kwa waimbaji wote iwe bongo fleva au dini, kipaimara, hatusi, sendoff na matukio mengineyo.

Kwa mawasiliano zaido tupigie simu namba
0762795251
0653795251

TUNAPATIKANA NJOMBE NDANI YA UWANJA WA SABASABA


BAADA YA KUONEKANA NA KIDOA HOTELINI;SAMATTA AWA MBOGO AFUNGUKA MAZITO KWA KIDOA AMSHANGAA KUTAFUTA UMAARUFU KUPITIA JINA LAKE,AFUNGUKA MAZITO JUU YA MREMBO HUYO NA GAZETI LA IJUMAA,ONA HAPA LIVEE



“Asha umekumbwa na nini na kwann unajaribu kufanya aya hao ijumaa ndo wamekufanya ufanye haya wanakulipa kiasi gani shemej yangu mbna tulikuwa tunaheshimiana sana inamaana iyo tuzo ya ijumaa sexiest girl ndo malipo yake kuwatafutia habar na habar iyo ujaona watu wengine mpk kwangu mm ambaye atuna ayo mazoea na kwa sababu gani ukaamua kunifanya ivi kama ulikuwa na matatizo ungeniambia nikusaidie sio kunitendea ivi unataka kupata nini zaidi najua ulipanga kila kitu ndo maana ulilazimisha kupiga picha na mimi na kulazimisha nikubebe kwny gar kumbe ndo lengo lako ilo umeamua kunipeleka kwny magazeti ya udaku kwa interest za nani na umepewa kiasi gani kuwatafutia iyo stor iv unajua wameingiza kiasi gani kwa ilo hongera bana Ila mm siwez kumfanyia ivi rafiki yangu asante sana mungu atalipa hili. Na nyie ijumaa inamaana iyo tuzo mlimpa uyu mtoto muwe munamtumia kupata habar zenu sio ok hongereni sana mungu atajaalia gazeti lenu liwe namba moja.nakunja goti nasali kwako shemeji yangu asha ujiitae kidoa na pia kwenu gazeti la ijumaa lengo lenu limefanikiwa mbarikiwe.samahanini wana michezo ili suala sio la kweli na limeniuma sana ndo maana nimeliweka apa” amesema Samatta


HATARIII;MWIGULU NNCHEMA ATOA UJUMBE HUU MKALI MARA BAADA YA KUMFUMA KIGOGO 'AKIPEPESA MACHO' NA PEMBEJEO ZA WAKULIMA


Ufuatiliaji wa Ugawaji wa pembejeo kwa wakulima,Nimefika wilaya ya Tunduru,Kata ya Nandembo na kata jirani kwaajili ya kujiridhisha na namna ugawaji wa pembejeo unavyofanyika kwa wakulima. Nimekutana na mchezo mchafu wa ugawaji wa pembejeo unaohusisha wakala wa pembejeo kula njama na viongozi wa serikali wa kata na vijiji kuwasainisha wakulima kuwa wamepokea pembejeo(Mbegu +Mbolea) ilia hali pembejeo hizo zinaishia mifukoni mwa wakala.Baadhi ya wakulima ambao sio waaminifu wanadiriki kupokea fedha kidogo iliwamuachie wakala zile pembejo akauze sehemu nyingine kwa bei ya juu ili hali ni ruzuku iliyotolewa na serikali kwaajili ya kuwasaidia wakulima kuboresha kilimo chao. Kwa hatua za awali kwa ubadhilifu uliofanywa na Uongozi wa kata ya Nandembo na mawakala waliopewa dhamana kusambaza pembejeo hizo wote wamekamatwa na jumatatu kupitia Kamati ya Ulinzi ya wilaya watapandishwa kizimbani.Lakini kuanzia sasa wakala Bw.Zuberi Namahala na Bw.Ibrahim Mohamed Ibrahim mbali ya kukamatwa na kufikishwa mahakamani,kuanzia sasa wamefutwa kwenye orodha ya mawakala wa pembejo. Natoa rai kwa Viongozi,Mawakala wa pembejeo na wakulima wote popote walipo kuhakikisha lengo la serikali la kuinua sekta ya Kilimo inafanyika kwa uaminifu na ufanisi,kwa yeyote yule anayeshiriki kuhujumu na kujinufaisha kupitia pembejeo zinazotolewa na serikali hatakwepa mkono wa serikali.

MBUNGE WA CCM MH NEEMA MGAYA AMWAGA MSAADA SHULE ZA MBEYELA NA SOVI MKOANI NJOMBE


Mhe .neema mgaya mbunge wa viti maalum akichangia vitabu 700 katika shule ya sekondari mbeyela iliyoko njombe mjini na shule ya sekondari sovi iliyopo jimbo la lupembe mkoani njombe.

TANZANIA KUKUMBWA NA MAFURIKO KUTOKANA NA MVUA ZA EL-NINO KATI YA JANUARI NA MARCHI MWAKA HUU.


UMOJA wa Mataifa umeihadharisha Tanzania kuwa itakumbwa na mafuriko yatakayosababishwa na mvua za El-Nino na kutaka kuanza kuchukua tahadhari mapema. 

Taarifa ya Umoja huo ya uwezekano mkubwa wa mafuriko yatakayosababishwa na mvua za El- Nino imetolewa wakati serikali inaendelea kubomoa nyumba zilizojengwa maeneo hatarishi katika mabonde na maeneo yasiyoruhusiwa. 

Kwa mujibu wa taarifa ya Katibu Mkuu Msaidizi Mwandamizi anayehusika na Misaada ya Kibinadamu na Uratibu wa Misaada ya Dharura, Stephen O’Brien, Tanzania inaweza kukabiliwa na mafuriko ya El-Nino kati ya mwezi huu wa Januari na Machi, mwaka huu. 

Pamoja na Tanzania, nchi nyingine ambazo zimetajwa kukumbwa na mafuriko hayo makubwa ni pamoja na Madagascar, Malawi na Msumbiji. 


Taarifa ya O’Brien kuhusu madhara ya El-Nino na namna gani Jumuiya ya Kimataifa inatakiwa kujiandaa au inajiandaa na kadhia hiyo iliwasilishwa mbele ya wajumbe wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa na nakala yake kutumwa kwa Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa. 

Pamoja na kutoa tahadhari hiyo, O’Brien amezisihi nchi ambazo zinatarajiwa kukumbwa na maafa ya El -Nino kujiandaa ipasavyo na kuyataja maandalizi hayo kuwa ni pamoja na utoaji wa misaada ya kibinadamu kwa wananchi watarajiwa wa athari za mvua hizo. 

Kwa mujibu wa Katibu Mkuu Msaidizi Mwandamizi, upande wa Afrika ya Mashariki, nchi kadhaa hususan ukanda wa magharibi zimekumbwa na uhaba mkubwa wa mvua na hivyo kuathiri kiwango cha upatikanaji wa chakula. 

Nchi hizo ni Ethiopia, Sudan, Djibouti na Eritrea ilihali baadhi ya nchi zikipata kiwango cha mvua kilichovuka mipaka. “ Kuanzia mwezi Januari hadi Machi, nchi za Tanzania, Msumbiji, Madagascar na Malawi zina uwezekano mkubwa wa kukumbwa na mafuriko ya El- Nino,” alisema O’Brien. 

Alisema nchi hizo zitahitaji pamoja na mambo mengine misaada ya kujiandaa na kushughulikia kile kinachotabiriwa kwani kina uwezekano mkubwa wa kutokea. 


Ukiacha nchi za Afrika ya Mashariki, nchi nyingine kwa upande wa Afrika ambazo zimekumbwa na hali tete ya uhaba wa mvua na hivyo kutishia usalama na upatikanaji wa chakula ni Angola, Botswana, Malawi, Namibia, Afrika Kusini, Swaziland, Zambia na Zimbabwe. 

O’Brien alisema nchi hizo zimekuwa na uhaba wa mvua kiasi kwamba zitakabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula na kusababisha watu zaidi ya milioni 28 katika mataifa hayo kukukosa chakula. 

Akizungumzia kuhusu misaada ambayo imekwishakutolewa na nchi wahisani ili kukabilia na ukame na madhara yatokanayo na El-Nino , Katibu Mkuu Msaidizi Mwandamizi huyo alisema kuwa hadi wakati anatoa taarifa yake kiasi cha Dola za Marekani milioni 360 kilikuwa kimetolewa na wafadhili kwa lengo la kukabiliana na madhara yatakayotokana na ElNino ikiwa ni pamoja na usalama wa chakula. 

Pamoja na michango hiyo, O’Brien alisema haitoshi kutokana na ukweli kwamba maafa yatakayotoka na madhila ya El-Nino yanahitaji misaada zaidi. 


Mbali ya nchi za kanda ya Afrika baadhi ya nchi nyingine ambazo zitakumbwa na zilishawahi kupata balaa la El-Nino ni pamoja na nchi ambao zimo katika Bara la Latini Amerika na nchi za eneo la Pasifiki ambazo nyingi ni visiwa. 

Shirika la Kimataifa la Hali ya Hewa (WMO) linatarajiwa Mwezi Februari kutoa taarifa zaidi kuhusu mwelekeo za mvua hizo za El-Nino. 


Mvua kama hizo zilishawahi kunyesha nchini Tanzania mwaka 1998 na kusababisha maafa makubwa na watu kadhaa walipoteza maisha, huku maelfu wengine wakijeruhiwa na kupoteza makazi. 

Mwaka jana mwezi Agosti Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) ilitoa tahadhari kuwa Tanzania ni kati ya nchi za Barani Afrika zitakazokumbwa na mvua za El Nino kati ya mwezi Septemba na Desemba, mwaka jana.HABARILEO

BREAKING NEWS : VIGOGO WENGINE BANDARI WANG'OLEWA ,UCHUNGUZI MKALI WAENDELEA


SERIKALI imeendelea kuisafisha Bandari kwa kuwaondoa watendaji wa ngazi za juu na kuwahamishia wizarani ili kuongeza ufanisi katika utendaji, sambamba na kuongeza ukusanyaji wa mapato.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam kuhusu mabadiliko Bandarini, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa 

Makame Mbarawa (pichani) alisema serikali ya awamu ya tano imedhamiria kuhakikisha inasimamia mapato ya serikali na taasisi zinafanya kazi kwa ufanisi mkubwa.
Aliwataja watumishi walioondolewa Bandari kuwa ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Peter Gawile, Kaimu Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), Killian Challe na Kaimu Mkurugenzi wa Manunuzi, Mashaka Kishanda.
Alisema watendaji hao wamerudishwa wizarani na itafanyika tathmini ili waangaliwe watapangiwa nafasi gani kwa kuwa inawezekana katika Bandari uwezo wao na ufanisi wao ulikuwa mdogo ila inawezekana maeneo mengine wakafanya vizuri zaidi.
Aidha alisema imewateua watendaji wengine kushika nafasi hizo akiwemo Anthony Mbilinyi kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ambaye anakwenda Bandari kushika nafasi ya Gawile, Benito Kalinga ambaye alikuwa Ofisa Manunuzi Mkuu wa TCRA anayeenda Bandari kushika nafasi ya Kishanda na Abdulrahaman Bamba ambae alikuwa TEHAMA Uchukuzi anayeenda kushika nafasi ya Challe.
“Tatizo kubwa lililokuwa linaonekana pale Bandari ni mfumo wa IT hivyo tumeamua hao waondoke… Tunaamini tukiwapa ushirikiano watendaji hawa wanaoingia watafanya vizuri zaidi na kufanikisha azma ya serikali ya kuongeza ukusanyaji wa mapato,” alisema.
Katika hatua nyingine, Profesa Mbarawa amemsimamisha kazi Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Charles Chacha na kutaka kuhamishwa mara moja kwa Mhasibu Mkuu Alhaji Said Mteule na Meneja manunuzi wa taasisi hiyo, Said Kaswela kwa kushindwa kusimamia ukusanyaji wa mapato katika taasisi hiyo.
Serikali pia imeona ifanye uchunguzi kuhusu ununuzi wa mtambo wa kufuatilia vyombo angani unaojulikana kama Automatic Data Surveillance-Broadcast (ADS-B) na mtambo wa kukusanya taarifa za usafiri wa anga (AMHS), ambayo imegharimu kiasi cha Euro milioni 1.5.
Mbarawa alitoa agizo hilo jana akiwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango pamoja na watendaji wa TCAA katika ziara aliyoizungumzia kuwa ni ya kuangalia uendeshaji na ukusanyaji wa mapato unavyofanyika katika taasisi hiyo.
Waziri huyo alisema kuna mambo yamejitokeza hivyo serikali imeona lazima ifanye uchunguzi kwenye ununuzi wa baadhi ya mitambo na pia imebaini kuna upotevu mkubwa wa ukusanyaji wa mapato ambao umechangiwa na uongozi wa taasisi kwa kutojipanga vizuri.
“Wizara imeamua Chacha kuanzia leo (jana), hataendelea na nafasi hiyo tena badala yake atatafutwa mwingine. Mhasibu Mkuu wa taasisi hii atahamishwa na ofisa wa manunuzi wa taasisi hii. Iko haja ya kumpeleka sehemu nyingine ili tupate mtu safi na makini,” alisema Waziri huyo.
Mitambo hiyo ilitakiwa kuanza kufanya kazi tangu Novemba mwaka jana, lakini mpaka sasa haijaanza kufanya kazi. “Bora ubaki na watu wawili kwenye kazi kuliko 10 ambao sio waadilifu,” alisema Mbarawa.
Kwa upande wake Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Mpango alisema kikubwa wanachopigania ni kuhakikisha serikali inakusanya mapato yote ya kodi na yasiyo ya kodi na kuongeza kuwa taasisi hiyo ina vyanzo ambavyo vingeweza kuingizia serikali fedha nyingi.
“Mkaguzi Mkuu alikuja na kufanya utafiti lakini taarifa aliyoitoa haikufanyiwa kazi. Pia katika kudodosa inajulikana TCAA ina akaunti saba ambazo zinatia shaka,”alisema Waziri Mpango na kuagiza akaunti hizo kutokuguswa mpaka uchunguzi utakapofanyika.
“Nimeagiza ili fedha za taasisi hii zibaki salama isitoke hata senti, pia ndani ya wiki mbili ufanyike ukaguzi kubaini upotevu wote wa fedha za umma uliofanyika,” alisema na kuitaka Mamlaka ya Usimamizi wa Manunuzi ya Umma (PPRA), ifanye uchunguzi wa mchakato mzima wa ununuzi wa mitambo hiyo miwili ya ADSB na AMHS, pamoja na kusisitiza kuwa watumishi waliosimamishwa watahamishwa mara moja.

CHANZO: HABARI LEO
 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU