ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

BREAKING NEWZZ:AJALI YA YAUA WATU WANNE DODOMA

Wednesday, December 21, 2016


Watu wanne wakiwamo polisi wawili, wamefariki dunia baada ya gari walilokuwa wakisafiria kuacha njia na kupindua katika kijiji cha Seruka kata ya Chipogoro tarafa ya Rudi wilayani Mpwapwa mkoa wa Dodoma.

Ajali hiyo ilitokea Desemba 19, mwaka huu, saa 11:30 jioni katika kijiji hicho baada ya gari walilokuwa wakisafiria T517 CDL Toyota Alphat katika barabara kuu ya Dodoma- Iringa, kuacha njia na kupinduka na kusababisha vifo vya watu wanne na majeruhi tisa.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani humo, Ernest Kimola, amesema gari hiyo iliyokuwa ikiendeshwa na Aggrey Lucas, baada ya kufika katika kijiji hicho, liliacha njia na kupinduka na kusababisha vifo vya askari Konstebo Mahende na Konstebo Sasi Mwita ambaye ni askari mkoa wa Songwe.

Kamanda Kimola amewataja wengine waliofariki katika ajali hiyo ni mke wa Konstebo Mwita, Pendo Mwita na Emaculata Nyangi.

Amewataja majeruhi wa ajali hiyo ni Neema Mwita (8), Jenifa Mwita (4), Nyangi Wambura (23), Konstebo Nashon (23) ambaye ni polisi kituo cha Tunduma na Baraka Chacha (9).

Wengine ni Juli Mwita (6), Pc Enock ambaye ni mmiliki wa gari lililopata ajali, Makongoro Charles na Elizabeth Cosmas ambao wote wamelazwa katika hospitali ya mkoa wa Dodoma.


Aidha, kamanda Kimola amesema miili ya marehemu hao waliofariki katika ajali hiyo, imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya mkoa wa Dodoma

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU