ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

Mahakama Misri yabatilisha hukumu ya vifo

Wednesday, February 3, 2016

wafuasi wa Muslim brotherhood
Wafuasi wa kundi lililopigwa marufuku la Muslim Brotherhood wakiwa gerezani
Mahakama nchini Misri imefuta hukumu ya kifo dhidi ya wafuasia 149 wa kundi lililopigwa marufuku la Muslim Brotherhood na kuamuru ianzishwe tena.
Watu hao walipatikana na hatia ya kufanya mashambulizi dhidi ya polisi mwaka 2013 kwenye kituo cha polisi cha Kerdasa, karibu na mji mkuu Cairo, ambapo polisi wapatao 11 waliuawa.
Misri ilifanya msako mkali dhidi ya wanamgambo wa kiislam tangu jeshi lilipomg'oa madarakani rais Mohammed Morsi mnamo mwaka 2013.
Mamia ya wafuasi wake wamekua wakihukumiwa kifo katika kesi zinazohusisha watu wengi.
Wanajeshi wa Misri
Wanajeshi wa Misri walivamia kambi ya waandamanaji wa Muslim Brotherhood wakati wa harakati za kudai mageuzi
Kesi hizo zilizua ukosoaji mkubwa kutoka kwa makundi ya haki za kibinadamu pamoja na Umoja wa Mataifa.
Morsi, ambae anatoka vugu vugu la Muslim Brotherhood, aliondolewa madarakani baada ya maandamano makubwa dhidi ya utawala wake
Tarehe 14 Agosti 2013,vikosi vya usalama vya Misri viliwavamia waandamanaji waliokua kwenye kambi zilizoandaliwa na wafuasi wa Muslim Brotherhood, na kusababisha vifo vya mamia ya watu.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU