ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

KANISA LACHOMWA MOTO SHINYANGA BAADA YA VIONGOZI WA KANISA KUTUMBULIWA JIPU

Thursday, February 25, 2016



Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Mika Nyange 

Kanisa la True Jesus lililopo katika  kijiji cha Igalamya kata ya Usule tarafa ya Samuye wilaya ya Shinyanga limechomwa moto na watu wasiojulikana kutokana na kile kinachodaiwa kuwa baadhi ya viongozi kanisa hilo walitumbuliwa jipu kwa kusimamishwa kuhudumu katika kanisa hilo.
 Kwa mujibu wa taarifa ya kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Mika Nyange  kwa vyomba vu ahabari tukio hilo limetokea Februari 22 mwaka huu saa sita usiku. 

Kamanda Nyange amesema chanzo cha tukio hilo ni baadhi ya viongozi wa kanisa hilo lililoezekwa kwa nyasi kusimamishwa kuhudumu katika kanisa hilo kutokana na kuwakaribisha wageni kutoka Kenya katika kanisa hilo bila kufuata utaratibu. 


Akifafanua zaidi Kamanda Nyange amesema kwa mujibu wa Askofu wa kanisa hilo Albinus Kichele viongozi waliosimamishwa kuhudumu katika kanisa hilo ni mwinjilisti wa kanisa Yona Nkuba na wainjilisti na walimu wa kanisa ambao ni John Peter,Jackson Bundala na Thereza Salamba. 
 Amesema kutokana na wageni hao kuingia bila kufuata utaratibu wa kanisa wageni hao walikamatwa na idara ya uhamiaji mkoa wa Shinyanga kisha kurudishwa kwao Kenya hali iliyosababisha viongozi hao wa kanisa kujitoa kwenye kanisa hilo kabla hawajasimamishwa. 

Kamanda Nyangi alisema jeshi la polisi mkoani Shinyanga linaendelea kufanya uchunguzi juu ya tukio hilo. 

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU