ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

HABARI MPYAAAA..................Kingunge Kuzikwa Jumatano Makaburi ya Kinondoni...........

Friday, February 2, 2018

Kingunge Kuzikwa Jumatano Makaburi ya Kinondoni

Mwanasiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombale-Mwiru anatarajiwa kuzikwa Jumatatu Februari 5, 2018 katika makaburi ya
Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa kamati ya maziko ya mwanasiasa huyo, Omary Kimbau amesema  Kingunge atazikwa saa tisa alasiri.

Hata hivyo, amesema leo Ijumaa Februari 2,2018 kuwa utaratibu na mipango mingine inaendelea kufanyika.

Kingunge amefariki dunia leo alfajiri akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).

Alikuwa akiuguza majeraha baada ya kung'atwa na mbwa mwishoni mwa mwaka jana nyumbani kwake.

Mpwa wa Kingunge, Tony Mwiru amesema familia inapitia kipindi kigumu kwa kuwa hivi karibuni wamempoteza mama yao, Peras.

Enock Mwiru ambaye ni mdogo wa marehemu na mtangazaji wa zamani wa iliyokuwa Redio Tanzania (RTD),  amesema  Kingunge alikuwa kiunganishi cha familia.

Mabalozi Juma Mwapachu na Ali Mchumo waliowahi kufanya kazi na Kingunge wamefika nyumbani kwa marehemu Kijitonyama kuhani msiba huo.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU