ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

Kiongozi 'aliyeidhinisha' kiapo cha Raila Odinga akamatwa

Friday, February 2, 2018

Wakili Miguna Miguna alihusika pakubwa katika kumlisha kiapo cha kuwa 'rais wa wananchi' kiongozi wa Nasa Raila Odinga
Mwanasiasa aliyejitangaza kuwa kiongozi wa vuguvugu la pingamizi dhidi ya serikali nchini Kenya NRM Miguna Miguna alikamatwa siku ya Ijumaa alfajiri, muda mfupi baada ya
kupiga kamsa kufuatia uvamizi wa polisi katika nyumba yake iliopo katika makaazi ya Runda jijini Nairobi.
Mkurugenzi wa kitengo cha ujasusi nchini Kenya George Kinoti alithibitisha kwamba bwana Miguna alikamatwa kwa kutoa kiapo kinyume na sheria mbali na kuwa mwanachama wa vuguvugu la NRM lililopigwa marufuku linalohisishwa na muungano wa Nasa.
''Bwana Miguna alitangaza hadharani kwamba yeye ndio jenerali wa vuguvugu hilo, ambalo tayari limetangazwa kuwa kundi haramu.Wakati alipotangaza hadharani kulikuwa na notisi ya gazeti rasmi la serikali iliotolewa na waziri''.
''Tutamuachaje sisi ni maafisa wa polisi'', alisema Kinoti.
''Pia alisema kwamba atawaongoza watu kuchoma picha za rais Uhuru aliyechaguliwa kidemokrasia.Sasa munatarajia nini kutoka kwetu''?.
''Pia alikiri kwamba ni yeye aliyeongoza kiapo hicho''.
Duru za maafisa wa polisi zimethibitisha kuwa bwana Miguna alipelekwa katika kituo cha polisi cha Kiambu kabla ya kuondolewa na kupelekwa eneo lisilojulikana.
Mapema bwana Miguna alimwambia muhariri wa gazeti la Nation kwamba maafisa wa polisi walivamia nyumba yake mapema alfajiri na kuipekuapekua .
Kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga baada ya kujiapisha kuwa rais wa wananchi katika bustani ya Uhuru park jijini NairobiHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionKiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga baada ya kujiapisha kuwa rais wa wananchi katika bustani ya Uhuru park jijini Nairobi
Wakili huyo ambaye alikuwa kiungo muhimu katika kumuapisha kiongozi wa Nasa Raila Odinga siku ya Jumanne katika uwanja wa Uhuru Park jijini Nairobi alithibitisha uvamizi huo katika ujumbe uliotumwa saa moja na robo alfajiri Ijumaa.
''Maafisa wa polisi walitumia bomu kuvunja na kuingia katika nyumba yangu. Siwezi kuzungumza katika simu hivi sasa. Wamepekua nyumba yangu'', alisema.
''Wengine wamejificha nje ya nyumba yangu wakitumai nitatoka ili waweze kunipiga risasi na kudai kwamba kulikuwa na ufyatulianaji wa risasi. Sitoki ng'o''.
Majirani walisema kuwa magari kadhaa yalikuwa katika nyumba ya Miguna mapema saa kumi na mbili alfajiri, lakini magari hayo baadaye yakaondoka.
Wafuasi wa Miguna walikuwa wameanza kujaa nje ya nyumba yake na baada ya dakika tano maafisa wa polisi walidaiwa kurusha vitoa machozi ili kuwatawanya.
Wafuasi hao walitoroka na kutazama kwa mbali huku magari ya polisi yaliombeba Miguna yakiondoka.
Baada ya maafisa wa polisi kuondoka , waandishi wa habari waliweza kuingia ndani, na hakukuwa na ishara yoyote ya Miguna huku nyumba hiyo ikiwachwa bila mtu.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU