ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

MCT YAMPONGEZA RAIS MAGUFULI KWA KUPAMBANA NA RUSHWA NA UBADHIRIFU

Tuesday, September 6, 2016


Wapili kutoka kushoto mstari wa kwanza ni mkurugunzi wa chuo cha uandishi wa habari cha Eckros Ndugu Erick Mlelwa

BARAZA la Habari Tanzania (MCT) limeipongeza serikali ya Rais John Magufuli kwa jitihada zake za kupambana na rushwa pamoja na ubadhirifu na kusema inapaswa kuungwa mkono na kila mmoja na pia vyombo vya habari. 

Katibu Mtendaji wa MCT, Kajubi Mukajanga alitoa pongezi hizo jana wakati wa
Mkutano Mkuu wa 18 wa Baraza hilo uliofanyika jijini Dar es Salaam. 

Mukajanga alisema kwa kuwa vyombo vya habari ni namba moja katika kupambana na rushwa, wanaiomba serikali itafute suluhu pale vinapokosea badala ya kuvifungia. 

“Midhali serikali inajua sheria zilizopo zinahitaji marekebisho, tupunguze kuzitumia kwa sababu hazitupeleki mbele, bali zinaturudisha nyuma,” alisema Mukajanga. 

Alisema hivi sasa Kamati ya Maadili ya Baraza hilo ambayo Mwenyekiti wake ni Jaji Juxon Mlay inaendelea kukusanya ushahidi wa kutosha ili waende kuzungumza na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye kuhusu mgogoro huo wa kuvifungia vyombo vya habari. 

Vyombo vya habari vilivyofungiwa na serikali hivi karibuni ni gazeti la Mseto na vituo vya redio vya Magic FM na Radio Five. Naye Rais wa baraza hilo, Jaji Thomas Mihayo alivitaka vyombo vya habari pamoja na waandishi wa habari visiogope kutumia haki yao ya msingi pale inapotokea wanavunjiwa uhuru wao wa kujieleza kwa sababu mahakama ni sehemu sahihi ya kudai haki kamili. 

“Watanzania wengi hawapendi kutumia vyanzo sahihi vya kuweza kupata haki yao. Waandishi wa habari mnapotaka kupata haki yenu nendeni mahakamani kwa sababu ni chombo cha pekee kinachoweza kutoa haki ya kweli," alisema Jaji Mihayo. 

Mbunge wa Ubungo kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa gazeti la MwanaHalisi, Said Kubenea alisema kuna tatizo kwa waandishi wa habari kuwa wavivu katika kutafuta haki mahakamani, pengine ni kutokana na mchakato mrefu. 

Aliiomba MCT kuwa mstari wa mbele katika kuzisimamia kesi hizo mahakamani, kwa kuwa kwa kufanya hivyo kutaipa kesi hizo nguvu. 

“Ni rai yangu MCT, lisimame katika kutetea waandishi na vyombo vya habari," alisema Kubenea. Katika hilo, Mukajanga alisema hilo ni jukumu lao wamelipokea hivyo watatenga fedha kwa ajili ya kusaidia uhuru wa habari nchini.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU