ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

Swansea yaichapa Liverpool 3-1

Monday, May 2, 2016


Andre Ayew akifunga bao la pili dhidi ya Liverpool

Mshambulizi wa Black Stars ya Ghana Andre Ayew alifunga mabao mawili na kuisadia timu yake ya Swansea kujihakikishia nafasi katika ligi kuu ya Uingereza msimu ujao.
Ayew alifunga mabao hayo Swansea City ilipojifurukuta na kuiadhibu Liverpool 3-1.
Ayew alifungua kibano hicho kwa mkwaju wa kichwa kabla ya Jack Cork kufuma kimiani mkwaju ulioipa swansea uongozi wa mabao mawili kwa nunge kufikia muda wa mapumziko.
Hata hivyo vijana wa Jurgen Klopp walirejea uwanjani kwa kishindo.
Christian Benteke alirejeshea Liverpool matumaini kwa kufunga bao mapema katika kipindi cha pili.
Lakini Ayew akawazimia nuru kabisa katik mechi hii alipofunga bao lake la tatu na la ushindi dakika mbili tu baadaye kunako dakika ya 67.
Masaibu ya Liverpool yaliongezeka Brad Smith alipooneshwa kadi yake ya pili ya njano na hivyo kulazimika kuiaga mechi hiyo.
Kufuatia kichapo hicho Liverpool sasa haina budi kujinga ukanda iliangalau waweze kushinda kombe la Europa iwapo bado wanamatumaini ya kushiriki katika kombe la mabingwa barani ulaya mwakani.
Kwa upande wao Swansea, ambao wanaorodhewshwa katika nafasi ya 13 wamejizolea alama 11 zaidi ya Sunderland ambayo iko katika hatari kubwa ya kushushwa daraja msimu ujao.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU