ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

HUU NDIO MWAKA AMBAO SERIKALI ITATOA MILIONI 50 KWA KILA KIJIJI.

Tuesday, May 3, 2016

Huu ndio mwaka ambao Serikali itaanza kutoa milioni 50 kila kijiji.

Serikali imesema itaanza kutekeleza ahadi ya Rais John Magufuli ya kukipa kila kijiji nchini Sh milioni 50  katika mwaka wa fedha wa 2016-2017.
Kauli hiyo ilitolewa bungeni jana na Naibu Waziri Ofisi ya Rais Sera, Uratibu, Bunge la Walemavu, Antony Mavunde alipojibu swali la  Mbunge wa Viti Maalumu, Halima Bulembo.
Bulembo alitaka kujua   ahadi ya Sh milioni 50 kwa kila kijiji itatekelezwa lini.
Mavunde alisema ahadi ya Rais Magufuli ya kila kijiji kupewa Sh milioni 50 itaanza kutekelezwa  katika mwaka wa fedha wa 2016-2017.
Alisema utaratibu wa kugawa fedha hizo unaandaliwa na Baraza la Uwezeshaji Wananchi kwa kushirikiana na Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.
‘’Pamoja na mikakati yote hiyo vigezo ambavyo vimekuwa vikitumika katika kutoa mikopo  na mitaji  kwa vijana ni umri usiozidi miaka 35 ambavyo  ni kujiunga na Saccos za vijana za wilaya na kuunda vikundi na kuvisajili kisheria,” alisema.
Alisema ili kuhakikisha vijana wanakuwa wajasiriamali na wanaweza kupatiwa mikopo na mitaji, serikali imejiwekea mikakati ya kutambua vijana na mahitji yao katika ngazi mbalimbali  na kutoa mafunzo ya ujasiriamali kwa makundi mbalimbali ya vijana.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU