ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

Rais wa Sao Tome na Principe asusia uchaguzi

Monday, August 8, 2016

Pinto da Costa
Katika hatua ya kushangaza, kiongozi wa visiwa vya Sao Tome na Principe, mojawapo ya mataifa madogo zaidi barani Afrika, amesusia awamu ya pili ya uchaguzi nchini humo.
Rais Manuel Pinto da Costa amesema uchaguzi huo hauwezi kuwa
wa haki na akawahimiza wafuasi wake kutoshiriki.
Aliwataka wafuasi wake kutoshiriki uchaguzi huo wa Jumapili baada ya kupata chini ya robo ya kura zilizopigwa katika duru ya kwanza.
Rais huyo alipata 24.8% ya kura zilizopigwa katika awamu hiyo ya kwanza tarehe 17 Julai naye mpinzani wake Evaristo Carvalho akapata 49.8%. Alisema uchaguzi huo wa kwanza ulikumbwa na udanganyifu.
Wafuasi wa Evaristo Carvalho
Taarifa zinasema wengi wa wafuasi wake walisusia uchaguzi huo wa kwanza.
Bw Carvalho, ambaye alikuwa spika wa bunge na pia waziri mkuu, anaonekana kuhakikishiwa ushindi.
Bw Pinto da Costa ameongoza kwa miaka mitano.
Awali, aliongoza taifa hilo wakati wa utawala wa chama kimoja kuanzia 1975 hadi 1991 alipofanikisha kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi.
Taifa hilo, ambalo lilitawaliwa na Ureno, linajumuisha visiwa viwili vikubwa Sao Tome na Principe pamoja na visiwa vingine vidogo.

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU