ECKROS SCHOOL OF JOURNALISM

eckroscollege. Powered by Blogger.

Blogroll

About

Habari za Mahusiano Kila siku

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

JOURNALISM STUDENTS AT ETC COLLEGE

ETC RADIO ONLINE LIVE

http://wwweckrosnewsblogspo.radio12345.com/

HABARI YA HIVI PUNDE: WAALIMU WAPYA WALIOPO NYUMBANI SASA KUNEEMEKA KWA AJIRA

Thursday, August 25, 2016


KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa imeomba Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa imuombe Rais atoe kibali cha ajira kwa walimu kukabili uhaba unaoikabili nchi.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Jasson Rweikiza alitoa ushauri huo jana mjini Dodoma kwenye kikao kati ya wajumbe wa kamati hiyo na viongozi na watendaji wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa wakiongozwa na Naibu Waziri, Selemani Jafo.

Kikao hicho kilikuwa ni cha kamati kupokea na kujadili taarifa ya tathmini ya utekelezaji wa mpango wa ofisi hiyo wa utoaji elimu bila malipo katika kipindi cha Januari hadi Juni mwaka huu ambako suala la uhaba wa walimu liliibuliwa na wajumbe.

“Walimu waajiriwe...ni vyema mumuone rais, angalau afungulie kibali cha walimu pekee...wanafunzi wanaongezeka mara mbili, lakini walimu hakuna,” alisema Rweikiza.

Awali, akijibu hoja za wajumbe juu ya changamoto ya uhaba wa walimu, hususan wa Sayansi na Hisabati, Jafo alikiri hali hiyo kuikumba serikali na kusema ndiyo maana walilenga kutoa ajira 35,000 kabla ya rais kusimamisha vibali vya ajira kwa watumishi wote.

Hata hivyo, alisema uamuzi wa Rais ni wa nia njema kuwezesha uhakiki wa watumishi hewa.

Alisema katika kauli ya hivi karibuni ya Rais John Magufuli, alisema wakati wowote kibali kitatolewa.

Jafo alisisitiza kuwa kibali kitakapotolewa, kipaumbele itakuwa ni ajira kwa walimu wa Sayansi ya Hisabati.


Akielezea namna ya kuziba mapengo ya walimu wa masomo hayo, Jafo alisema serikali itafikiria pia watu wengine wanaoweza kufaa katika kufundisha masomo hayo wakiwemo walimu wastaafu na wahitimu wa fani nyingine. 

No comments:

Post a Comment

 

Most Reading

Eckros Computer Lap 1

Eckros Computer Lap 1

About ETC College

Eckros Tourism College (ETC) started admitting the first intake of students in January 2013. The college falls under tertiary higher education and training as stipulated in education and training policy of 1995.
Also the college administer Distance Learning Programmes, Evening classes, weekend classes, study tours and researchs programmes
Admission Process
New admission into the College is effected twice a year in January-July and July-December.

WALIO PITIA BLOG YETU