Muhammad Yussuf
Katika Gazeti la NIPASHE toleo la Jumaane tarehe 20 Desemba 2016, kulichapishwa makala yenye kichwa cha maneno “CCM yarudisha kivingine staili ya uvuaji magamba”. Pamoja na mambo mengine, Mwandishi wa makala hiyo,Thobias Mwanakatwe, aliandika kama hivi:
“CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimesema matajiri wenye mikono michafu inayohusika na rushwa na dhuluma, wakae kando na chama hicho kwa kuwa kimeanza safari ya


